ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - فهرس التراجم


ترجمة معاني سورة: الضحى   آية:

سورة الضحى - Surat Ad-Duha

وَٱلضُّحَىٰ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa dhuha, na uliokusudiwa ni wakati wa mchana mzima.
التفاسير العربية:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku utuliapo na viumbe na likashadidi giza lake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Atakacho katika viumbe vyake. Ama kiumbe, hafai kuapa kwa asiyekuwa Muumba wake. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
التفاسير العربية:
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Hakukuwacha Mola wako, ewe Mtume, wala Hakukuchukia kwa kuchelewesha kukuteremshiaWahyi.
التفاسير العربية:
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na Nyumba ya Akhera ni bora kwako kuliko nyumba ya ulimwengu.
التفاسير العربية:
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Atakupa Mola wako, ewe Mtume, neema ya kila sampuli uridhike.
التفاسير العربية:
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani Hakukupata, kabla ya hapo, kuwa ni yatima Akakukusanya na kukutunza.
التفاسير العربية:
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na Akakupata hujui Kitabu wala Imani, Akakufundisha yale amabayo ulikuwa huyajui na akakuafikia kufanya amali bora?
التفاسير العربية:
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Na Akakupata masikini, Akakuletea riziki yako na Akakutajirisha kwa kutosheka na kusubiri?
التفاسير العربية:
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimtende ubaya.
التفاسير العربية:
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na muombaji usimkaripie, bali mlishe na umtimizie haja yake.
التفاسير العربية:
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na ama neema ya Mola wako Aliyokuneemesha nayo izungumze.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني سورة: الضحى
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

إغلاق