የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ ዐበሰ   አንቀጽ:

Surat Abasa

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Yalidhihiri mabadiliko na mkunjiko katika uso wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ
na akapa nyongo kwa sababu ya kwamba Abdallah bin Ummi Maktum alimjilia akitaka aelekezwe. Na alikuwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ameshughulika kuwalingania miamba wa Kikureshi katika Uislamu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Ni kitu gani kinakufanya wewe ujue uhakika wa jambo lake? Kwani huenda ikawa, kwa kuuliza kwake, nafsi yake itatakasika na kusafika.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ
Au pengine apate mazingatio zaidi na kutishika.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ
Basi yule alijyejitosheleza na kutouhitajia uongozi wako,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
wewe ndiye unayemjali na wapulikiza maneno yake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na ni kitu gani kinachokupa jukumu kwako iwapo hakusafika na ukafiri wake?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ
Ama yule ambaye amekuwa na pupa la kukutana na wewe,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَهُوَ يَخۡشَىٰ
na huku anamuogopa Mwenyezi Mungu asiwe na kasoro katika kupata uongofu,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ
wewe unampuuza. Ilivyotakikana ufanye si kama ulivyofanya, ewe Mtume.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ
Hakika Sura hii ni mawaidha kwako na kwa kila anayetaka kuwaidhika.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi atakaye atamkumbuka Mwenyezi Mungu na kumtaja na atafuata Wahyi Wake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ
Wahyi huu, nao ni Qur’ani, uko katika kurasa zilizotukuzwa,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ
zenye kuheshimiwa, zenye cheo cha juu,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ
zilizosafishwa na uchafu, uongezaji na upunguzaji.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كِرَامِۭ بَرَرَةٖ
Zilizoko mikononi mwa Malaika waandishi, mabalozi kati ya Mwenyezi Mungu na viumbe Wake, wenye maumbile mema, tabia zao ni nzuri na njema na pia matendo yao.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ
Amelaaniwa mtu kafiri na ataadhibiwa. Ni uovu ulioje wa ukafiri wake kwa Mola wake!
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Kwani hajui ni kwa kitu gani Mwenyezi Mungu Alimuumba kwacho mwanzo wake?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Mwenyezi Mungu Alimuumba kwa maji machache, nayo ni manii. Akayakadiria miongo yake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha Akambainishia njia ya kheri na ya shari.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ
Kisha humkosesha uhai, na Amemuekea mahali pa kuzikiwa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha Akitaka Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na sifa mbaya, Atamhuisha na kumfufua baada ya kifo chake, kwa ajili ya kuhesabiwa na kulipwa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ
Mambo siyo kama yale anayoyasema kafiri na anayoyafanya. Bado hajatakeleza Aliyomuamrisha kwayo Mwenyezi Mungu katika kuamini na kutenda wema kwa kumtii.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Na azingatie binadamu, vipi Mwenyezi Mungu Amekiumba chakula chake ambacho ndicho kinachoendeleza maisha yake?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Aone kwamba Sisi Tumeyamimina maji ya mvua juu ya ardhi kwa wingi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Kisha Tumeipasua ardhi kwa Tulivyo vitoa kutoka humo miongoni mwa mimea tofauti.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Tukaotesha humo nafaka
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
na zabibu, na nyasi za wanyama.Na mizaituni na mitende.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mabustani yenye miti mikubwa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na matunda
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
na ndisha.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Mnajistareheshea kwazo, nyinyi na wanyama wenu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Utakapokuja Ukelele wa Siku ya Kiyama, ambao utayatia uziwi, kwa kitisho chake, masikizi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku mtu atakapomkimbia, kwa kitisho cha Siku Hiyo, nduguye
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
na babake na mamake na
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
mkewe na wanawe.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
Kila mmoja Siku Hiyo, atakuwa na jambo litakalomzuia asishughulike na mwingine.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Nyuso za wenye neema, Siku Hiyo, zitakuwa ni zenye kung’ara,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
zenye furaha na nderemo.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na nyuso za watu wa Motoni zitakuwa na giza,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
nyeusi, zafinikwa na unyonge.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao wenye kusifika na sifa hiyo ndiwo wale waliozikufuru neema za Mwenyezi Mungu na wakazikanusha aya zake na wakayakeuka Aliyoyaharamisha kwa kutenda maovu na kukiuka mipaka.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ ዐበሰ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዶ/ር ሙሐመድ ዓብደሏህ አቡ በክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ

መዝጋት