የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አል ሙጠፊፊን   አንቀጽ:

Surat Al-Mutaffifin

وَيۡلٞ لِّلۡمُطَفِّفِينَ
Adhabu kali ni ya wale wanaopunja vipimo vya vibaba na mezani.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكۡتَالُواْ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسۡتَوۡفُونَ
Ambao wakinunua kwa watu cha kupimwa kwa vibaba au kwa mizani hujikamilishia wao wenyewe.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَإِذَا كَالُوهُمۡ أَو وَّزَنُوهُمۡ يُخۡسِرُونَ
Na wakiwauzia watu kinachouzwa kwa vibaba au mizani wanapunguza vipimo.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَلَا يَظُنُّ أُوْلَٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبۡعُوثُونَ
Basi itakuwaje hali ya yule anayeiba na kupunja katika vipimo vyote hivyo, au yule anayeiba katika vipimo hivyo na huku awapunja watu vitu vyao? Hakika huyo yuwastahiki mateso zaidi kuliko wapunguzaji wa vipimo vya vibaba na mizani. Kwani hawaamini wale wapunjaji ya kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mwenye kuwafufua na kuwahesabu juu ya vitendo vyao.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لِيَوۡمٍ عَظِيمٖ
katika Siku itakapokuwa na kitisho?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
يَوۡمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Siku watakaposimama watu mbele ya Mweyezi Mungu ili Awahesabu kwa machache na mengi walioyatenda, hali ya kuwa wao Siku Hiyo ni wenye kumnyenyekea Mwenyezi Mungu, Mlezi wa viumbe vyote.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٖ
Hakika marejeo ya watu waovu na makazi yao yatakuwa katika hali ya dhiki.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سِجِّينٞ
Na ni kipi kinachokujulidha dhiki hii ni ipi?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ
Hakika hiyo itakuwa ni jela ya kudumu na adhabu iliyo na uchungu. Penye jela hiyo ni pale walipoandikiwa kuwa watakwenda. Wameandikiwa na imepitishwa. Hapana kitakachozidishwa wala kupunguzwa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Adhabu kali Siku Hiyo ni ya wale wenye kukanusha.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
Wale ambao wanakanusha kuwako tukio la Siku ya Malipo.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ
Na wala haikanushi Siku Hiyo isipokuwa kila dhalimu mwenye madhambi mengi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Anaposomewa aya za Qur’ani, husema, «Hizi ni hadithi za urongo za watu wa kale.» Mambo yalivyo si kama wanavyodai!
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّاۖ بَلۡۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ
Bali hayo ni maneno ya Mwenyezi Mungu na Wahyi Wake kwa Mtume Wake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّآ إِنَّهُمۡ عَن رَّبِّهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّمَحۡجُوبُونَ
Na hakika zimezibwa nyoyo zao zikawa hazimkubali Mwenyezi Mungu. Na kile kilichoziziba nyoyo hizo ni kufinikwa na wingi wa madhambi wanayoyafanya. Mambo hayako kama vile wanavyodai makafiri! Bali hakika wao, Siku ya Kiyama watazibwa wasimuone Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda. Aya hii ni ushahidi kwamba Waumini watamuona Mola Wao Peponi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ إِنَّهُمۡ لَصَالُواْ ٱلۡجَحِيمِ
Kisha hakika hao makafiri ni wenye kuingia Motoni, na wataziona na kuzihisi dharubu zake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Kisha wataambiwa,»Haya ndiyo malipo ya yale ambayo mlikuwa mnayakanusha.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡأَبۡرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ
Ni kweli kabisa kwamba kitabu cha watu wema, nao ni wachamungu, kiko katika ngazi za juu Peponi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ
Na ni kipi kinachokujulisha ni zipi hizi ngazi za juu?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ
Ni kitabu cha watu wema kilichopitishwa mambo yake, hakizidishwi kitu humo wala hakipunguzwi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
يَشۡهَدُهُ ٱلۡمُقَرَّبُونَ
Wanayatazama yaliyomo ndani yake Malaika waliokurubishwa, wa kila mbingu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٍ
Hakika wale wenye ukweli na kufuata amri za Mwenyezi Mungu watakuwa Peponi wnaneemeka,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
juu ya viti vya fahari wanamwangalia Mola wao na wanaangalia yale waliyoandaliwa miongoni mwa kheri nyingi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
تَعۡرِفُ فِي وُجُوهِهِمۡ نَضۡرَةَ ٱلنَّعِيمِ
Unaonekana katika nyuso zao mng’aro wa neema.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
يُسۡقَوۡنَ مِن رَّحِيقٖ مَّخۡتُومٍ
Watanyweshwa tembo safi, lililotengezewa vyombo kwa ustadi na mwishowe kuna harufu ya miski.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
خِتَٰمُهُۥ مِسۡكٞۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلۡيَتَنَافَسِ ٱلۡمُتَنَٰفِسُونَ
Katika kuzipata neema hizo, nawashindane wenye kushindana.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسۡنِيمٍ
Na kinywaji hiki, mchanganyo wake watokana na chemchemi iliyoko Peponi linalojulikana, kwa ubora wake, kwa jina la Tasnīm.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
عَيۡنٗا يَشۡرَبُ بِهَا ٱلۡمُقَرَّبُونَ
Hiyo ni chemchemi iliyoandaliwa wale waliokurubishwa kwa Mwenyezi Mungu na watajiburudisha nayo.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجۡرَمُواْ كَانُواْ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ يَضۡحَكُونَ
Hakika wale waliotenda maovu walikuwa duniani wakiwacheza shere Waumini.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَإِذَا مَرُّواْ بِهِمۡ يَتَغَامَزُونَ
Na wanapowapitia wanakonyezana kwa kuwakejeli.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓاْ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِمُ ٱنقَلَبُواْ فَكِهِينَ
Na wnaporudi, hawa waovu, kwa watu wao na jamaa zao, huwa na vihunzi na wao kwa kuwafanyia maskhara Waumini.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَإِذَا رَأَوۡهُمۡ قَالُوٓاْ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ
Na hawa makafiri wanapowaona Maswahaba wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, wamefuata uongofu, huwa wakisema, «Hakika hawa wamepotea kwa kumfuata Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَمَآ أُرۡسِلُواْ عَلَيۡهِمۡ حَٰفِظِينَ
Na wala waovu hawa hawakutumwa wawe ni wachunguzi kwa Maswahaba na Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَٱلۡيَوۡمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنَ ٱلۡكُفَّارِ يَضۡحَكُونَ
Basi Siku ya Kiyama wale waliomkubali Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakafanya vitendo vinavyolingana na sheria Zake, watawafanyia maskhara makafiri kama makafiri walivyokuwa wakiwafanyia mashara duniani.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
Juu ya viti vya fahari, watakuwa Waumini wanaangalia yale Aliyowapa Mwenyezi Mungu miongoni mwa mambo matukufu na neema, wakiwa Peponi. Na neema kubwa ya zote ni kuangalia Uso wa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
هَلۡ ثُوِّبَ ٱلۡكُفَّارُ مَا كَانُواْ يَفۡعَلُونَ
Je, wamelipwa makafiri, pindi watakapo kufanyiwa hayo, malipo muwafaka na yale waliyoyafanya duniani ya shari na madhambi?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አል ሙጠፊፊን
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዶ/ር ሙሐመድ ዓብደሏህ አቡ በክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ

መዝጋት