የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አል አዕላ   አንቀጽ:

Surat Al-A'la

سَبِّحِ ٱسۡمَ رَبِّكَ ٱلۡأَعۡلَى
Takasa Jina la Mola wako Aliyetukuka na kuepukana na mshirika na kila sifa pungufu kwa namna inayonasibiana na utukufu Wake na utakatifu Wake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ٱلَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ
Aliyeumba viumbe Akalitengeneza umbo lao na kulifanya zuri.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱلَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ
Na Aliyekadiria kila kitu na kukipeleka njia inayonasibiana nacho.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلۡمَرۡعَىٰ
Na Aliyeotesha nyasi mbiti zenye rangi ya kijani,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحۡوَىٰ
Akazifanya baadaye kuwa kavu zilizobadilika rangi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
سَنُقۡرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ
Tutakusomea, ewe Mtume, hii Qur’ani kisomo ambacho hutakisahau.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ
Isipokuwa iwapo Mwenyezi Mungu Ataka usahau kwa hekima na maslahi anayoyajua Yeye. Kwani Yeye ni Mjuzi wa yaliyo wazi na yaliyofichika, ya maneno na ya vitendo.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَنُيَسِّرُكَ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutakufanyia mapesi mambo yako yote; miongoni mwayo ni kukusahilishia kubeba majukumu ya utume na kuifanya nyepesi Dini uliyokuja nayo.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ
Basi wawaidhie kaumu zako, ewe Mtume, kwa namna tulivyokutayarishia ufanye kwenye wahyi ulioletewa, uwaongoze njia yenye kheri na wao na uwahusu kwa mawaidha yako wale wanaotarajiwa kuwaidhika nayo. Wala usijisumbue kuwashauri wale ambao mawidha hayawaathiri isipokuwa kuwatia ujeuri na kuwafanya wayakimbie.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخۡشَىٰ
Atanufaika kwa mawaidha anayemcha Mola wke,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلۡأَشۡقَى
na atajiepusha na mawaidha aliye mbaya asiyemuogopa Mola wake
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ٱلَّذِي يَصۡلَى ٱلنَّارَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
atakayeingia kwenye Moto wa Jahanamu akiadhibika kwa ukali wake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ
Kisha hatakuwa ni mwenye kufa akapumzika wala ni mwenye kuishi akanufaika.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ
Hakika amefuzu mwenye kuisafisha nafsi yake na tabia mbovu,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَذَكَرَ ٱسۡمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ
na akamtaja Mwenyezi Mungu, akampwekesha, akamuomba, akafanya vitendo vya kumridhisha na akasimamisha Swala kwa nyakati zake kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu na kufuata sheria Aliyoiweka.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
بَلۡ تُؤۡثِرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Hakika yenu, nyinyi watu, mnafadhilisha pambo la maisha ya kilimwengu juu ya starehe za Akhera.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ وَأَبۡقَىٰٓ
Na hakika ya mambo ni kuwa nyumba ya Akhera na starehe zake ni bora zaidi kuliko ulimwngu na ni yenye kusalia zaidi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّ هَٰذَا لَفِي ٱلصُّحُفِ ٱلۡأُولَىٰ
Haya mlioosimuliwa ndani ya Sura hii ni miongoni mwa yaliyotajwa kimaana katika Kurasa zilizotangulia kuteremshwa kabla ya Qur’ani.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
صُحُفِ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ
Nazo ni Kurasa za Ibrāhīm na Mūsā, amani ziwashukie.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አል አዕላ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዶ/ር ሙሐመድ ዓብደሏህ አቡ በክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ

መዝጋት