የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አል በለድ   አንቀጽ:

Surat Al-Balad

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mji huu mtakatifu wa Makkah.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Na wewe, ewe Nabii, ni mkazi wa mji huu mtakatifu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ
Na Anaapa kwa mzazi wa wanaadamu, ambaye ni Ādam, amani imshukie, na kilichozalikana na yeye.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ
Hakika Tumemuumba binadamu katika usumbufu na shida za kilimwengu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ
Kwani anadhani kwa mali aliyoyakusanya kuwa Mwenyezi Mungu Hatakuwa na uwezo juu yake?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا
Huwa akisema kwa kujigamba: «Nimetumia mali mengi.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Kwani anadhani, kwa kitendo chake hiko, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda, Hamuoni wala hatamhesabu juu ya kubwa na dogo?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ
Kwani hatukumpa macho mawili ya kuonea,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ
ulimi na midomo miwili ya kusemea
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ
na kumfafanulia njia mbili: ya kheri na ya shari?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ
Basi ajiepushe na janga la Akhera kwa kutoa mali yake ili aokoke.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ
Ni kitu gani kilichojulisha ni lipi hilo janga la Akhera na ni mambo gani yenye kusaidia kujiepusha nalo?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَكُّ رَقَبَةٍ
Ni kuacha huru shingo iliyoamini kuikomboa na utumwa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ
Au kulisha, wakati wa shida ya njaa,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ
yatima mwenye ujamaa, ili ipatikane fadhila ya sadaka na ya kuunga kizazi,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ
au masikini asiyekuwa na kitu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ
Kisha akawa, baada ya kufanya amali njema zilizotajwa, ni miongoni mwa waliotakasa Imani yao kwa Mwenyezi Mungu, wakausiana kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu kwa kufuata maamrisho Yake na kujiepusha na vitendo vya kumuasi na wakausiana kuwahurumia viumbe.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Wenye kufanya hayo ndiwo watu wa kulia ambao watapelekwa Siku ya Kiyama upande wa kulia kuelekea Peponi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Na wale waliokanusha Qur’ani ndio ambao watapelekwa, Siku ya Kiyama, upande wa kushoto kuelekea Motoni.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ
Malipo yao ni Moto wa Jahanamu wenye kuwafinika na kuwaziba.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አል በለድ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዶ/ር ሙሐመድ ዓብደሏህ አቡ በክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ

መዝጋት