ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (19) سورة: يونس
وَمَا كَانَ ٱلنَّاسُ إِلَّآ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ فَٱخۡتَلَفُواْۚ وَلَوۡلَا كَلِمَةٞ سَبَقَتۡ مِن رَّبِّكَ لَقُضِيَ بَيۡنَهُمۡ فِيمَا فِيهِ يَخۡتَلِفُونَ
Wala watu hawakuwa ila Umma mmoja tu. Kisha wakakhitalifiana. Na lau kuwa si neno lililo kwisha tangulia kutokana na Mola wako Mlezi, hapana shaka hukumu ingeli kwisha katwa baina yao katika hayo wanayo khitalifiana.
Watu kwa maumbile yao hawakuwa ila ni Umma mmoja tu. Kisha tukawapelekea Mitume wawaongoze na wawaongoe kwa mujibu wa Ufunuo wa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Ikawa tabia ya kibinaadamu iliyo pelekea kheri na shari ndiyo sababu ya kuwa na nguvu zaidi shari katika baadhi yao. Juu yao hao matamanio na nyendo za Shetani zikatawala, na kwa hivyo wakakhitalifiana. Na lau kuwa hukumu ya Mola wako Mlezi haikutangulia ya kuwapa muhula makafiri kwa ajili yako, Ewe Nabii, na kuakhirisha maangamizo yao mpaka siku maalumu iliyo ahidiwa, Mwenyezi Mungu angeli wapelekea upesi maangamizo na adhabu, kwa sababu ya mfarakano waliyo uingia, kama zilivyo ingia kaumu zilizo kwisha pita.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (19) سورة: يونس
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق