ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (77) سورة: يوسف
۞ قَالُوٓاْ إِن يَسۡرِقۡ فَقَدۡ سَرَقَ أَخٞ لَّهُۥ مِن قَبۡلُۚ فَأَسَرَّهَا يُوسُفُ فِي نَفۡسِهِۦ وَلَمۡ يُبۡدِهَا لَهُمۡۚ قَالَ أَنتُمۡ شَرّٞ مَّكَانٗاۖ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا تَصِفُونَ
Wakasema: Ikiwa huyu ameiba, basi nduguye vile vile aliiba zamani. Lakini Yusuf aliyaweka siri moyoni mwake wala hakuwaonyesha. Akawaambia: Nyinyi mko katika hali mbaya zaidi, na Mwenyezi Mungu anajua zaidi hayo mnayo singizia.
Kule kugunduliwa kikopo katika mzigo wa ndugu yake kwa ghafla kuliwashangaza nduguze na kukawababaisha. Kwa hivyo wakataka kujivua kuwa wao wote hawana makosa ila huyo na Yusuf, na kusema kuwa tabia ya wizi wameirithi kwa mama yao. Wakasema: Si ajabu kuwa huyo kaiba, kwani nduguye khalisa aliwahi kwiba vile vile! Na Yusuf akatambua kijembe chao wanacho mpigia, na yakamuudhi hayo. Lakini aliyaficha, na akawawekea jawabu moyoni mwake lau kuwa amesema wazi jawabu yenyewe inge kuwa hivi: Nyinyi mko katika hali ovu zaidi, na nyinyi ni duni zaidi. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua vyema, na kutambua ukweli wa maneno yenu ya kumsingizia nduguye fedheha ya wizi.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (77) سورة: يوسف
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق