ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (35) سورة: النحل
وَقَالَ ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُواْ لَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ مَا عَبَدۡنَا مِن دُونِهِۦ مِن شَيۡءٖ نَّحۡنُ وَلَآ ءَابَآؤُنَا وَلَا حَرَّمۡنَا مِن دُونِهِۦ مِن شَيۡءٖۚ كَذَٰلِكَ فَعَلَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ فَهَلۡ عَلَى ٱلرُّسُلِ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ
Na washirikina wanasema: Mwenyezi Mungu angeli taka tusingeliabudu chochote badala yake, sisi wala baba zetu, wala tusingeli harimisha chochote bila ya Yeye. Kama hivyo walifanya walio kuwa kabla yao. Basi lipo lolote juu ya Mitume isipo kuwa kubalighisha kwa uwazi?
Na washirikina wakasema kwa inda na ukosefu: Lau kama Mwenyezi Mungu angeli penda tumuabudu Yeye tu peke yake na tumt'ii kwa anayo tuamuru, basi tusingeli muabudu mwenginewe, wala tusingeli harimisha sisi wenyewe kitu asicho harimisha Yeye kama Bahira na Saiba. Na hii ni hoja potovu wanayo itafutia njia katika ukafiri wao. Na makafiri walio kwisha tangulia walitoa hoja kama hizo, baada ya kuwapelekea Mitume wetu, wakaamrisha Tawhidi (kumuabudu Mwenyezi Mungu Mmoja), na kumt'ii Yeye, na wakawakataza ushirikina na kuharimisha asivyo harimisha Mwenyezi Mungu. Hoja ikasimama dhidi yao. Na Mitume wetu wakatimiza tuliyo waamrisha wayafikishe. Na juu yetu kuwahisabu wao. Na Mitume hawana jukumu zaidi ya hayo.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (35) سورة: النحل
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق