ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (92) سورة: النحل
وَلَا تَكُونُواْ كَٱلَّتِي نَقَضَتۡ غَزۡلَهَا مِنۢ بَعۡدِ قُوَّةٍ أَنكَٰثٗا تَتَّخِذُونَ أَيۡمَٰنَكُمۡ دَخَلَۢا بَيۡنَكُمۡ أَن تَكُونَ أُمَّةٌ هِيَ أَرۡبَىٰ مِنۡ أُمَّةٍۚ إِنَّمَا يَبۡلُوكُمُ ٱللَّهُ بِهِۦۚ وَلَيُبَيِّنَنَّ لَكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ مَا كُنتُمۡ فِيهِ تَخۡتَلِفُونَ
Wala msiwe kama mwanamke anaye uzongoa uzi wake baada ya kwisha usokota ukawa mgumu. Mnavifanya viapo vyenu kuwa ni njia ya kudanganyana baina yenu kwa kuwa ati taifa moja lina nguvu zaidi kuliko jengine? Hakika Mwenyezi Mungu anakujaribuni kwa njia hiyo. Na bila ya shaka atakubainishieni Siku ya Kiyama mliyo kuwa mkikhitalifiana.
Wala msiwe katika kwenda kinyume na viapo vyenu baada ya kuvithibitisha mfano wa mwanamke mwendawazimu anaye sokoto sufi, ikisha kuwa nyuzi akazifumua tena. Mkafanya viapo vyenu kuwa ni njia ya kudanganya na kukhadaa watu, na huku mkijitafutia udhuru kwa kuwa ama nyinyi ni wengi zaidi au mna nguvu zaidi kuliko wao, au mnakusudia kuwaunga mkono maadui wenye nguvu zaidi kuliko wao, au kwa kuwa mnataraji kuzidi nguvu kwa khiana! Na hakika Mwenyezi Mungu anakufanyieni mtihani. Mkikhiari kutimiza ahadi mtapata mavuno ya duniani na Akhera. Mkielekea khiana, basi ni khasara yenu. Na hakika Siku ya Kiyama atakubainishieni ukweli wa khitilafu zenu za duniani, na atakulipeni kwa mujibu wa vitendo vyenu. Aya mbili hizi zinaonyesha kuwa msingi wa makhusiano baina ya Waislamu na wengineo pamoja na uadilifu ni kutimiza ahadi, na kwamba makhusiano baina ya mataifa hayasimami sawa ila kwa kutimiza ahadi, na kwamba dola za Kiislamu zikijifunga kwa mapatano basi zijifunge kwa jina la Mwenyezi Mungu. Maana ya hayo ni kuwa inakuwapo yamini ya Mwenyezi Mungu na kuwa Yeye ndiye dhamini. Na Aya inafahamisha mambo matatu, ambayo lau kuwa mataifa yangeli yatimiza basi amani ingeli enea: Kwanza: Haifai mapatano kuwa ndio njia ya kufanya khadaa. Ikiwa hivyo inakuwa ni udanganyifu. Na udanganyifu haufai katika makhusiano baina ya wanaadamu, sawa sawa ikiwa baina ya mtu na mtu, au kikundi na kikundi, au baina ya madola. Pili: Kutimiza ahadi peke yake ni nguvu. Na mwenye kuvunja ahadi ni kama mwenye kuvunja alicho kijenga kwa sababu za nguvu. Basi anakuwa kama mpumbavu anaye tatua uzi wake kila akisha usokota. Tatu: Haimfalii mtu kuvunja ahadi kwa sababu ya kutafuta nguvu au kutaka kuzidisha kipande cha ardhi.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (92) سورة: النحل
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق