ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (144) سورة: آل عمران
وَمَا مُحَمَّدٌ إِلَّا رَسُولٞ قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِهِ ٱلرُّسُلُۚ أَفَإِيْن مَّاتَ أَوۡ قُتِلَ ٱنقَلَبۡتُمۡ عَلَىٰٓ أَعۡقَٰبِكُمۡۚ وَمَن يَنقَلِبۡ عَلَىٰ عَقِبَيۡهِ فَلَن يَضُرَّ ٱللَّهَ شَيۡـٔٗاۚ وَسَيَجۡزِي ٱللَّهُ ٱلشَّٰكِرِينَ
Na Muhammad hakuwa ila ni Mtume tu. Wamekwisha pita kabla yake Mitume. Je, akifa au akauwawa ndiyo mtageuka mrudi nyuma? Na atakaye geuka akarudi nyuma huyo hatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu atawalipa wanao mshukuru.
Katika vita vya Uhud ulitoka uvumi kuwa ati Mtume Muhammad s.a.w. kauwawa. Baadhi ya Waislamu walidahadari wakaingiwa kiwewe wakataka kurtadi, kuuacha Uislamu. Mwenyezi Mungu aliwakaripia kwa kuwaambia: Muhammad si chochote ila ni Mtume tu, na kabla yake wamekufa Mitume mfano wake yeye. Naye atakufa kama walivyo kufa wao, na atapita kama wao walivyo pita. Je, akifa au akauliwa ndio mtarejea nyuma kwenye ukafiri wenu? Na mwenye kurejea kwenye ukafiri baada ya kwisha amini, basi hatomdhuru kitu Mwenyezi Mungu, ila atakuwa anajidhuru nafsi yake kwa kujipeleka kwenye mateso. Na Mwenyezi Mungu atawalipa malipo mema wale wenye kusimama imara juu ya Uislamu, wenye kuishukuru neema yake.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (144) سورة: آل عمران
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق