ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (6) سورة: المائدة
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا قُمۡتُمۡ إِلَى ٱلصَّلَوٰةِ فَٱغۡسِلُواْ وُجُوهَكُمۡ وَأَيۡدِيَكُمۡ إِلَى ٱلۡمَرَافِقِ وَٱمۡسَحُواْ بِرُءُوسِكُمۡ وَأَرۡجُلَكُمۡ إِلَى ٱلۡكَعۡبَيۡنِۚ وَإِن كُنتُمۡ جُنُبٗا فَٱطَّهَّرُواْۚ وَإِن كُنتُم مَّرۡضَىٰٓ أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوۡ جَآءَ أَحَدٞ مِّنكُم مِّنَ ٱلۡغَآئِطِ أَوۡ لَٰمَسۡتُمُ ٱلنِّسَآءَ فَلَمۡ تَجِدُواْ مَآءٗ فَتَيَمَّمُواْ صَعِيدٗا طَيِّبٗا فَٱمۡسَحُواْ بِوُجُوهِكُمۡ وَأَيۡدِيكُم مِّنۡهُۚ مَا يُرِيدُ ٱللَّهُ لِيَجۡعَلَ عَلَيۡكُم مِّنۡ حَرَجٖ وَلَٰكِن يُرِيدُ لِيُطَهِّرَكُمۡ وَلِيُتِمَّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Enyi mlio amini! Mnapo simama kwa ajili ya Swala basi osheni nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake vichwa vyenu, na osheni miguu yenu mpaka vifundoni. Na mkiwa na janaba basi ogeni. Na mkiwa wagonjwa au mmo safarini, au mmoja wenu ametoka chooni au mmewagusa wanawake, na hamkupata maji, basi tayamamuni vumbi lilio safi, na mpake nyuso zenu na mikono yenu. Hapendi Mwenyezi Mungu kukutieni katika taabu; bali anataka kukutakaseni na kutimiza neema yake juu yenu ili mpate kushukuru.
Enyi Waumini! Mkitaka kuswali nanyi hamna udhu, tawadhini kwa kukosha nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake maji kichwa kizima au baadhi yake. Na mkoshe miguu yenu mpaka vifundoni. Mnapo taka kuswali nanyi mna janaba kwa kuingiliana na wake zenu, basi kogeni mwili mzima. Ikiwa mna maradhi ambayo hayakufaliini kutumia maji, au mpo safarini na ipo taabu ya maji, au mmetoka chooni kukidhi haja, au mmeingiliana (kwa lugha ya Qur'ani "kugusana") na wanawake na msipate maji, basi inakupaseni kutayamamu, yaani kujipaka vumbi lilio safi. Na hayo ni kwa kupangusa kwa hilo vumbi nyuso zenu na mikono yenu. Na Mwenyezi Mungu hataki kukudhikini katika hayo anayo kuamrisheni, bali anakupeni sharia za kukusafisheni ndani na nje, ili atimize neema zake juu yenu kwa uwongofu, na kubainisha na kusahilisha, mpate kumshukuru kwa uwongofu wake na kutimilia neema yake kwa kudumisha ut'iifu kwake. T'ahara (Usafi) wa Kiislamu una maana mbili: Moja ni kumwelekea Mwenyezi Mungu Mtukufu moyoni kwa kujiweka tayari kwa hayo, na kufunga azimio kusimama mbele yake na hali ni mwenye nafsi iliyo t'aahiri, na moyo ulio safi kabisa kwake Yeye tu. Pili ni unadhifu wa dhaahiri kwa udhu. Na katika hayo ni kuvikosha viungo vyote vinavyo weza kuchafuka. Na udhu ni jambo la kufanywa mara kwa mara, na huweza kufika hata kutwa mara tano. Pia kuna kukoga unapo ingiliana na mke, na wakati wa damu ya mwezi na uzazi. Udhu na kukoga ni kuondoa takataka zenye vijidudu vya maradhi, na pia huleta uchangamfu kwa kusisimua damu ya kwenye ngozi, na kupoza mishipa. Na kwa hivyo Mtume s.a.w. aliusia: "Ukihamaki tawadha".
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (6) سورة: المائدة
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق