ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (116) سورة: الأنعام
وَإِن تُطِعۡ أَكۡثَرَ مَن فِي ٱلۡأَرۡضِ يُضِلُّوكَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَإِنۡ هُمۡ إِلَّا يَخۡرُصُونَ
Na ukiwat'ii wengi katika hawa waliomo duniani watakupoteza na Njia ya Mwenyezi Mungu. Hawa hawafuati ila dhana tu, na hawakuwa ila ni wenye kusema uwongo tu.
Na ikiwa Subhanahu ndiye mwenye hukumu ya uadilifu inayo rejewa kwenye Vitabu vyake katika kutafuta Haki na kuijua, basi ewe Nabii, usiwe wewe na walio pamoja nawe, mkamfuata yeyote anaye achana na kauli ya Haki, hata ikiwa hao ni wengi wa idadi. Kwani ukiwafuata aghlabu ya watu ambao hawategemei Sharia iliyo teremshwa na Mwenyezi Mungu, watakuweka mbali na Njia ya Haki iliyo nyooka. Na hiyo ndiyo Njia ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na watu hao hawendi ila nyuma ya dhana na mawazo tu, na wala hawasemi ila kwa kukisia tu; hawategemei hoja na ushahidi.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (116) سورة: الأنعام
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق