ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني آية: (60) سورة: الأنفال
وَأَعِدُّواْ لَهُم مَّا ٱسۡتَطَعۡتُم مِّن قُوَّةٖ وَمِن رِّبَاطِ ٱلۡخَيۡلِ تُرۡهِبُونَ بِهِۦ عَدُوَّ ٱللَّهِ وَعَدُوَّكُمۡ وَءَاخَرِينَ مِن دُونِهِمۡ لَا تَعۡلَمُونَهُمُ ٱللَّهُ يَعۡلَمُهُمۡۚ وَمَا تُنفِقُواْ مِن شَيۡءٖ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ يُوَفَّ إِلَيۡكُمۡ وَأَنتُمۡ لَا تُظۡلَمُونَ
Basi waandalieni nguvu kama muwezavyo, na kwa farasi walio fungwa tayari-tayari, ili kuwatishia maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zenu, na wengineo ambao hamwajui, lakini Mwenyezi Mungu anawajua. Na mkitoa chochote katika Njia ya Mwenyezi Mungu mtarudishiwa, na wala nyinyi hamtadhulumiwa.
Enyi Umma wa Kiislamu! Tayarisheni kila muwezavyo nguvu za vita za namna zote kwa ajili ya kujizatiti kwa ajili ya kupigana, na wekeni askari walinzi na farasi wao mipakani na kando kando ya nchi, ili kwa hivi mjitayarishe na ulinzi mwatie kiwewe adui za Mwenyezi Mungu na adui zenu miongoni mwa hao makafiri ambao wamo kungojea likupateni jambo. Na pia mpate kuwatishia wenginewe ambao nyinyi hamwajui hivi sasa, lakini Mwenyezi Mungu anawajua, kwani hapana jambo linalo jificha kwake. Na kila mnacho kitoa kwa kuzitayarisha nguvu zenu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, basi Yeye atakulipeni malipo ya kutosha, bila ya kupunguka hata chembe katika mnayo stahiki katika fadhila ya Mola wenu Mlezi Katika Aya hii tukufu pana kuhimizwa na kuamrishwa kujitayarisha kwa ajili ya kupambana na adui. Kwani vita, zamani na sasa, ni jambo la khatari na muhimu kabisa. Juu yake inategemea kheri na shari, kufa kupona kwa umati na umati. Basi yapasa kujitayarisha, kujizatiti, na kujitengeneza kwa jiha mbali mbali za vifaa na silaha na zana. Kuingia vitani bila ya kujipatia zana zote na kujitayarisha ni kutafuta kushindwa. Na tunaona hivi sasa madola yanavyo jiandaa wakati wa amani na vita, na yanavyo jenga siasa zao na mipango yao na wanavyo kusanya uwezekano wao wote ili wapate ushindi katika vita. Na vita sasa havimsazi mtu. Wanashiriki katika vita wanajeshi na raia. Kwa hivyo ndio inapasa zaidi kujitengeneza kila mmoja wao kwa matengenezo ya kuwakusanya na kuwaweka tayari wote ili upatikane ushindi.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني آية: (60) سورة: الأنفال
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق