ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - فهرس التراجم

XML CSV Excel API
تنزيل الملفات يتضمن الموافقة على هذه الشروط والسياسات

ترجمة معاني سورة: الشرح   آية:

سورة الشرح - Surat Ash-Sharh

أَلَمۡ نَشۡرَحۡ لَكَ صَدۡرَكَ
Hatukukunjulia kifua chako?
Hakika tumekukunjulia kifua chako kwa kuwa tulitia ndani yake Uwongofu na Imani.
التفاسير العربية:
وَوَضَعۡنَا عَنكَ وِزۡرَكَ
Na tukakuondolea mzigo wako!
Na tumekupunguzia mizigo iliyo kuwa mizito juu ya mgongo wako, kwa kukuunga mkono na kukusahilishia mambo yako,
التفاسير العربية:
ٱلَّذِيٓ أَنقَضَ ظَهۡرَكَ
Ulio vunja mgongo wako?
Ambayo yalikuwa ni mazito juu ya mgongo wako.
التفاسير العربية:
وَرَفَعۡنَا لَكَ ذِكۡرَكَ
Na tukakunyanyulia utajo wako?
Na tumelitukuza jina lako, tukalifanya linatajwa na ulimi wa kila Muumini pamoja na jina letu.
التفاسير العربية:
فَإِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرًا
Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi!
Hizo ni baadhi ya neema zetu juu yako. Basi kuwa na yakini na uweza wa Mwenyezi Mtukufu, kwani pamoja na uzito upo wepesi mwingi unao kuja nao.
التفاسير العربية:
إِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرٗا
Hakika pamoja na uzito upo wepesi.
Hakika pamoja na uzito (wakati huo huo ijapo kuwa wewe hujui), upo wepesi mwingi vile vile.
التفاسير العربية:
فَإِذَا فَرَغۡتَ فَٱنصَبۡ
Na ukipata faragha, fanya juhudi.
Basi ukipata nafasi katika kazi ya kuwalingania watu, na mambo yaliyo khusiana na Jihadi, endelea na jitihada ya ibada na jishughulishe nafsi yako katika hayo.
التفاسير العربية:
وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَٱرۡغَب
Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.
Kwa Mola wako Mlezi tu ndio uelekee kwa kumwomba na kumhitajia.
التفاسير العربية:
 
ترجمة معاني سورة: الشرح
فهرس السور رقم الصفحة
 
ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - فهرس التراجم

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

إغلاق