আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - ছাৱাহিলী অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ আৰু নাচিৰ খামীছ * - অনুবাদসমূহৰ সূচীপত্ৰ


অৰ্থানুবাদ ছুৰা: ছুৰা আল-লাইল   আয়াত:

Surat Al-Lail

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa usiku unapoifinika ardhi na vilivyoko juu yake kwa giza lake.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Na kwa mchana unapofunuka mwangaza wake kutoka kwenye giza la usiku.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Na kwa kuumba mbea mbili: ya kiume na ya kike,
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
إِنَّ سَعۡيَكُمۡ لَشَتَّىٰ
Kuwa vitendo vyenu vinatofautiana: kuna wenye kufanyia dunia na wenye kufanyia Akhera.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فَأَمَّا مَنۡ أَعۡطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Ama mwenye kutoa kwenye mali yake, akamcha Mwenyezi Mungu katika huko kutoa,
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَصَدَّقَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
akaamini «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na Imani hiyo na akaamini malipo yanayofungamana nayo,
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutamuongoza na kumuafikia njia za kheri na wema na kumsahilishia mambo yake.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسۡتَغۡنَىٰ
Na ama mwenye kuyafanyia ubakhili mali yake, asiwe na haja ya malipo ya Mola wake,
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَكَذَّبَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
akakanusha neno la «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na neno hilo na akakanusha malipo yanayofungamana nalo,
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡعُسۡرَىٰ
Tutamnyoshea njia za mateso.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَمَا يُغۡنِي عَنۡهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ
Wala hayatamfaa yeye mali yake aliyoyafanyia ubakhili atakapotumbukia Motoni.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
إِنَّ عَلَيۡنَا لَلۡهُدَىٰ
Ni juu Yetu, kwa fadhila Zetu na busara Yetu, kueleza njia ya uongofu yenye kufikisha kwa Mwenyezi Mungu na ya upotevu.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَإِنَّ لَنَا لَلۡأٓخِرَةَ وَٱلۡأُولَىٰ
Na Sisi Tuna mamlaka ya maisha ya Akhera na maisha ya ulimwenguni.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فَأَنذَرۡتُكُمۡ نَارٗا تَلَظَّىٰ
Ndipo nikawaonya , enyi watu, na kuwatisha moto wenye kuwaka, nao ni moto wa Jahanamu.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
لَا يَصۡلَىٰهَآ إِلَّا ٱلۡأَشۡقَى
Hataingia Moto huo isipokuwa aliyekuwa mbaya sana. Mwenye kumkanusha Nabii Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
ٱلَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
na akakataa kumwamini na kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلۡأَتۡقَى
Na ataepushwa nao mchaji Mwenyezi Mungu sana.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
ٱلَّذِي يُؤۡتِي مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ
Ambaye hutoa mali yake kwa kutaka nyongeza za kheri
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعۡمَةٖ تُجۡزَىٰٓ
kutoa Kwake si kwa kulipa zema alizofanyiwa na mtu.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Lakini anatoa kwa kutaka uso wa Mola wake na radhi zake. Basi Mwenyezi Mungu atampa,
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَلَسَوۡفَ يَرۡضَىٰ
huko Peponi, malipo ya kumridhisha.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
 
অৰ্থানুবাদ ছুৰা: ছুৰা আল-লাইল
ছুৰাৰ তালিকা পৃষ্ঠা নং
 
আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - ছাৱাহিলী অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ আৰু নাচিৰ খামীছ - অনুবাদসমূহৰ সূচীপত্ৰ

ছাৱাহিলী ভাষাত কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ- অনুবাদ কৰিছে ড. আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ আবু বকৰ আৰু শ্বাইখ নাচিৰ খামীছ।

বন্ধ