আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - ছাৱাহিলী অনুবাদ- আলী মুহছিন আল-বিৰৱানী * - অনুবাদসমূহৰ সূচীপত্ৰ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

অৰ্থানুবাদ ছুৰা: ছুৰা আত-তীন   আয়াত:

Surat At-Tin

وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيۡتُونِ
Naapa kwa tini na zaituni!
Naapa kwa tini na zaituni, kwa baraka zao na ubora wa manufaa yao.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَطُورِ سِينِينَ
Na kwa Mlima wa Sinai!
Na kwa mlima ambao juu yake ndio Mwenyezi Mungu alimsemeza Musa.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ ٱلۡأَمِينِ
Na kwa mji huu wenye amani!
Na kwa huu mji mtukufu wa Makka, ambao anaushuhudia utukufu wake mwenye kwenda uzuru, na anapata amani mwenye kuuingia.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِيٓ أَحۡسَنِ تَقۡوِيمٖ
Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.
Kwa hakika bila ya shaka yoyote Sisi tumemuumba mtu amesimama sawa kwa umbo bora kabisa lilio nyooka, na akasifika kwa sifa nzuri kabisa.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
ثُمَّ رَدَدۡنَٰهُ أَسۡفَلَ سَٰفِلِينَ
Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
Kisha tukamteremsha cheo mpaka akawa ni wa chini kabisa katika hao walioko chini, kwa kuacha kufanya waajibu wa hayo tuliyo muumbia.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَلَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونٖ
Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.
Lakini walio amini na wakatenda vitendo vyema, hao basi watapata ujira usio wakatikia wala kuwapungukia.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعۡدُ بِٱلدِّينِ
Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?
Basi kitu gani kinacho kupelekea kukadhibisha kufufuliwa na kulipwa baada ya kuwekwa wazi uweza wetu wa hayo?
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَحۡكَمِ ٱلۡحَٰكِمِينَ
Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?
Kwani Mwenyezi Mungu aliye yatenda hayo tuliyo kueleza si muadilifu kuliko mahakimu wote kwa kufanya na kupanga?
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
 
অৰ্থানুবাদ ছুৰা: ছুৰা আত-তীন
ছুৰাৰ তালিকা পৃষ্ঠা নং
 
আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - ছাৱাহিলী অনুবাদ- আলী মুহছিন আল-বিৰৱানী - অনুবাদসমূহৰ সূচীপত্ৰ

ছাৱাহিলী ভাষাত কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ- অনুবাদ কৰিছে মুহছিন আল-বিৰৱানী

বন্ধ