Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis * - Tərcumənin mündəricatı


Mənaların tərcüməsi Surə: əl-Mutaffifin   Ayə:

Surat Al-Mutaffifin

وَيۡلٞ لِّلۡمُطَفِّفِينَ
Adhabu kali ni ya wale wanaopunja vipimo vya vibaba na mezani.
Ərəbcə təfsirlər:
ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكۡتَالُواْ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسۡتَوۡفُونَ
Ambao wakinunua kwa watu cha kupimwa kwa vibaba au kwa mizani hujikamilishia wao wenyewe.
Ərəbcə təfsirlər:
وَإِذَا كَالُوهُمۡ أَو وَّزَنُوهُمۡ يُخۡسِرُونَ
Na wakiwauzia watu kinachouzwa kwa vibaba au mizani wanapunguza vipimo.
Ərəbcə təfsirlər:
أَلَا يَظُنُّ أُوْلَٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبۡعُوثُونَ
Basi itakuwaje hali ya yule anayeiba na kupunja katika vipimo vyote hivyo, au yule anayeiba katika vipimo hivyo na huku awapunja watu vitu vyao? Hakika huyo yuwastahiki mateso zaidi kuliko wapunguzaji wa vipimo vya vibaba na mizani. Kwani hawaamini wale wapunjaji ya kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mwenye kuwafufua na kuwahesabu juu ya vitendo vyao.
Ərəbcə təfsirlər:
لِيَوۡمٍ عَظِيمٖ
katika Siku itakapokuwa na kitisho?
Ərəbcə təfsirlər:
يَوۡمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Siku watakaposimama watu mbele ya Mweyezi Mungu ili Awahesabu kwa machache na mengi walioyatenda, hali ya kuwa wao Siku Hiyo ni wenye kumnyenyekea Mwenyezi Mungu, Mlezi wa viumbe vyote.
Ərəbcə təfsirlər:
كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٖ
Hakika marejeo ya watu waovu na makazi yao yatakuwa katika hali ya dhiki.
Ərəbcə təfsirlər:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سِجِّينٞ
Na ni kipi kinachokujulidha dhiki hii ni ipi?
Ərəbcə təfsirlər:
كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ
Hakika hiyo itakuwa ni jela ya kudumu na adhabu iliyo na uchungu. Penye jela hiyo ni pale walipoandikiwa kuwa watakwenda. Wameandikiwa na imepitishwa. Hapana kitakachozidishwa wala kupunguzwa.
Ərəbcə təfsirlər:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Adhabu kali Siku Hiyo ni ya wale wenye kukanusha.
Ərəbcə təfsirlər:
ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
Wale ambao wanakanusha kuwako tukio la Siku ya Malipo.
Ərəbcə təfsirlər:
وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ
Na wala haikanushi Siku Hiyo isipokuwa kila dhalimu mwenye madhambi mengi.
Ərəbcə təfsirlər:
إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Anaposomewa aya za Qur’ani, husema, «Hizi ni hadithi za urongo za watu wa kale.» Mambo yalivyo si kama wanavyodai!
Ərəbcə təfsirlər:
كَلَّاۖ بَلۡۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ
Bali hayo ni maneno ya Mwenyezi Mungu na Wahyi Wake kwa Mtume Wake.
Ərəbcə təfsirlər:
كَلَّآ إِنَّهُمۡ عَن رَّبِّهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّمَحۡجُوبُونَ
Na hakika zimezibwa nyoyo zao zikawa hazimkubali Mwenyezi Mungu. Na kile kilichoziziba nyoyo hizo ni kufinikwa na wingi wa madhambi wanayoyafanya. Mambo hayako kama vile wanavyodai makafiri! Bali hakika wao, Siku ya Kiyama watazibwa wasimuone Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda. Aya hii ni ushahidi kwamba Waumini watamuona Mola Wao Peponi.
Ərəbcə təfsirlər:
ثُمَّ إِنَّهُمۡ لَصَالُواْ ٱلۡجَحِيمِ
Kisha hakika hao makafiri ni wenye kuingia Motoni, na wataziona na kuzihisi dharubu zake.
Ərəbcə təfsirlər:
ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Kisha wataambiwa,»Haya ndiyo malipo ya yale ambayo mlikuwa mnayakanusha.»
Ərəbcə təfsirlər:
كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡأَبۡرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ
Ni kweli kabisa kwamba kitabu cha watu wema, nao ni wachamungu, kiko katika ngazi za juu Peponi.
Ərəbcə təfsirlər:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ
Na ni kipi kinachokujulisha ni zipi hizi ngazi za juu?
Ərəbcə təfsirlər:
كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ
Ni kitabu cha watu wema kilichopitishwa mambo yake, hakizidishwi kitu humo wala hakipunguzwi.
Ərəbcə təfsirlər:
يَشۡهَدُهُ ٱلۡمُقَرَّبُونَ
Wanayatazama yaliyomo ndani yake Malaika waliokurubishwa, wa kila mbingu.
Ərəbcə təfsirlər:
إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٍ
Hakika wale wenye ukweli na kufuata amri za Mwenyezi Mungu watakuwa Peponi wnaneemeka,
Ərəbcə təfsirlər:
عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
juu ya viti vya fahari wanamwangalia Mola wao na wanaangalia yale waliyoandaliwa miongoni mwa kheri nyingi.
Ərəbcə təfsirlər:
تَعۡرِفُ فِي وُجُوهِهِمۡ نَضۡرَةَ ٱلنَّعِيمِ
Unaonekana katika nyuso zao mng’aro wa neema.
Ərəbcə təfsirlər:
يُسۡقَوۡنَ مِن رَّحِيقٖ مَّخۡتُومٍ
Watanyweshwa tembo safi, lililotengezewa vyombo kwa ustadi na mwishowe kuna harufu ya miski.
Ərəbcə təfsirlər:
خِتَٰمُهُۥ مِسۡكٞۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلۡيَتَنَافَسِ ٱلۡمُتَنَٰفِسُونَ
Katika kuzipata neema hizo, nawashindane wenye kushindana.
Ərəbcə təfsirlər:
وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسۡنِيمٍ
Na kinywaji hiki, mchanganyo wake watokana na chemchemi iliyoko Peponi linalojulikana, kwa ubora wake, kwa jina la Tasnīm.
Ərəbcə təfsirlər:
عَيۡنٗا يَشۡرَبُ بِهَا ٱلۡمُقَرَّبُونَ
Hiyo ni chemchemi iliyoandaliwa wale waliokurubishwa kwa Mwenyezi Mungu na watajiburudisha nayo.
Ərəbcə təfsirlər:
إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجۡرَمُواْ كَانُواْ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ يَضۡحَكُونَ
Hakika wale waliotenda maovu walikuwa duniani wakiwacheza shere Waumini.
Ərəbcə təfsirlər:
وَإِذَا مَرُّواْ بِهِمۡ يَتَغَامَزُونَ
Na wanapowapitia wanakonyezana kwa kuwakejeli.
Ərəbcə təfsirlər:
وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓاْ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِمُ ٱنقَلَبُواْ فَكِهِينَ
Na wnaporudi, hawa waovu, kwa watu wao na jamaa zao, huwa na vihunzi na wao kwa kuwafanyia maskhara Waumini.
Ərəbcə təfsirlər:
وَإِذَا رَأَوۡهُمۡ قَالُوٓاْ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ
Na hawa makafiri wanapowaona Maswahaba wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, wamefuata uongofu, huwa wakisema, «Hakika hawa wamepotea kwa kumfuata Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Ərəbcə təfsirlər:
وَمَآ أُرۡسِلُواْ عَلَيۡهِمۡ حَٰفِظِينَ
Na wala waovu hawa hawakutumwa wawe ni wachunguzi kwa Maswahaba na Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Ərəbcə təfsirlər:
فَٱلۡيَوۡمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنَ ٱلۡكُفَّارِ يَضۡحَكُونَ
Basi Siku ya Kiyama wale waliomkubali Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakafanya vitendo vinavyolingana na sheria Zake, watawafanyia maskhara makafiri kama makafiri walivyokuwa wakiwafanyia mashara duniani.
Ərəbcə təfsirlər:
عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
Juu ya viti vya fahari, watakuwa Waumini wanaangalia yale Aliyowapa Mwenyezi Mungu miongoni mwa mambo matukufu na neema, wakiwa Peponi. Na neema kubwa ya zote ni kuangalia Uso wa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Ərəbcə təfsirlər:
هَلۡ ثُوِّبَ ٱلۡكُفَّارُ مَا كَانُواْ يَفۡعَلُونَ
Je, wamelipwa makafiri, pindi watakapo kufanyiwa hayo, malipo muwafaka na yale waliyoyafanya duniani ya shari na madhambi?
Ərəbcə təfsirlər:
 
Mənaların tərcüməsi Surə: əl-Mutaffifin
Surələrin mündəricatı Səhifənin rəqəmi
 
Qurani Kərimin mənaca tərcüməsi - Səvahili dilinə tərcümə - Abdullah Məhəmməd və Nasir Xamis - Tərcumənin mündəricatı

Qurani Kərimin səvahili dilinə mənaca tərcüməsi. Tərcümə etdilər: Dr. Abdullah Muhəmməd Əbu Bəkr və Şeyx Nəsr Xamis.

Bağlamaq