কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ - সোয়াহিলি ভাষায় অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ ও নাসির খামীস * - অনুবাদসমূহের সূচী


অর্থসমূহের অনুবাদ সূরা: সূরা আর-রাহমান   আয়াত:

Surat Ar-Rahman

ٱلرَّحۡمَٰنُ
mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema
আরবি তাফসীরসমূহ:
عَلَّمَ ٱلۡقُرۡءَانَ
Amemfundisha binadamu Qur’ani kwa kurahisisha kuisoma, kuihifadhi na kuelewa maana yake.
আরবি তাফসীরসমূহ:
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ
Amemuumba binadamu,
আরবি তাফসীরসমূহ:
عَلَّمَهُ ٱلۡبَيَانَ
Amemfundisha ufasaha wa kujieleza ili kumtenganisha na wengine.
আরবি তাফসীরসমূহ:
ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ بِحُسۡبَانٖ
Jua na mwezi zinatembea kwa kufuatana, moja baada ya nyingine, kwa hesabu madhubuti isiyotafautiana wala kugongana.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلنَّجۡمُ وَٱلشَّجَرُ يَسۡجُدَانِ
Na nyota iliyo mbinguni na miti ya ardhini, vinamjua Mola wao, vinamsujudia na vinanyosha shingo zao kufuata vile ambavyo vimepangiwa vifuate vya maslahi ya waja Wake na manufaa yao.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلسَّمَآءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ ٱلۡمِيزَانَ
Na mbingu Ameiinua na kuifanya iwe juu ya ardhi, Na Ameweka kwenye ardhi uadilifu Aliouamrisha na kuulazimisha kwa waja Wake.
আরবি তাফসীরসমূহ:
أَلَّا تَطۡغَوۡاْ فِي ٱلۡمِيزَانِ
Ili msipite mipaka na msimfanyie hiyana mnayempimia.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَأَقِيمُواْ ٱلۡوَزۡنَ بِٱلۡقِسۡطِ وَلَا تُخۡسِرُواْ ٱلۡمِيزَانَ
Na simamisheni upimaji kwa usawa na msipunguze mizani mnapowapimia watu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلۡأَرۡضَ وَضَعَهَا لِلۡأَنَامِ
Na ardhi Ameiweka na Ameitayarisha, ili viumbe vitulie juu yake.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فِيهَا فَٰكِهَةٞ وَٱلنَّخۡلُ ذَاتُ ٱلۡأَكۡمَامِ
Humo mna matunda na mitende yenye makarara ya matunda. Na humo kuna nafaka zenye maganda, vikiwa ni chakula chenu na wanyama wenu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلۡحَبُّ ذُو ٱلۡعَصۡفِ وَٱلرَّيۡحَانُ
Na humo mna kila mmea wenye harufu nzuri.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Bas ni neema gani za Mola wenu, za kidini na za kidunia, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha? Na ni jawabu nzuri ilioje ya majini alipowasomea wao Nabii, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, sura hii, kila akipita kwenye aya hii walikuwa wakisema, «Hakuna chochote miongoni mwa neema zako, ewe Mola wetu, tunachokanusha. Sifa njema zote ni zako.» Na hivi ndivyo inavyotakiwa kwa mja anapoelezewa neema za Mwenyezi Mungu na mema Yake akubali na amshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema hizo.
আরবি তাফসীরসমূহ:
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٖ كَٱلۡفَخَّارِ
Amemuumba baba wa wanadamu, naye ni Ādam, kwa udongo mkavu kama vyungu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَخَلَقَ ٱلۡجَآنَّ مِن مَّارِجٖ مِّن نَّارٖ
Na Amemuumba Iblisi, naye ni katika majini, kwa mroromo wa moto uliochanganyika.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقَيۡنِ وَرَبُّ ٱلۡمَغۡرِبَيۡنِ
Mola wa pande mbili za Mashariki ya jua, katika kusi na kaskazi, na Mola wa pande mbili za Magharibi ya jua, katika kusi na kaskazi, kwani vyote viko chini ya uendeshaji Wake na ulezi Wake..
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
مَرَجَ ٱلۡبَحۡرَيۡنِ يَلۡتَقِيَانِ
Mwenyezi Mungu Ameyachanganya maji ya bahari mbili, tamu na chumvi, yanakutana, baina yake kuna kizuizi,
আরবি তাফসীরসমূহ:
بَيۡنَهُمَا بَرۡزَخٞ لَّا يَبۡغِيَانِ
mojawapo haiingii sehemu ya nyingine na kuiondoa sifa yake, bali ya tamu inasalia kuwa tamu na ya chumvi inasalia kuwa chumvi pamoja na kukutana kwake.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
يَخۡرُجُ مِنۡهُمَا ٱللُّؤۡلُؤُ وَٱلۡمَرۡجَانُ
Inatoka kwenye bahari mbili hizo, kwa uweza wa Mwenyezi Mungu, lulu na marjani.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَلَهُ ٱلۡجَوَارِ ٱلۡمُنشَـَٔاتُ فِي ٱلۡبَحۡرِ كَٱلۡأَعۡلَٰمِ
Ni Yake Yeye, Aliyetakasika na kutukuka, mamlaka ya kuyaendesha majahazi makubwa yanayotembea baharini kwa manufaa ya watu, yenye kusimamisha juu milongoti yake na matanga yake kama vile majabali.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
كُلُّ مَنۡ عَلَيۡهَا فَانٖ
Kila aliye juu ya uso wa ardhi miongoni mwa viumbe ni mwenye kuangamia,
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَيَبۡقَىٰ وَجۡهُ رَبِّكَ ذُو ٱلۡجَلَٰلِ وَٱلۡإِكۡرَامِ
na utasalia uso wa Mola wako Mwenye utukufu, ubora, kheri nyingi na upaji. Katika aya hii pana kuthibitisha sifa ya uso kwa Mwenyezi Mungu kwa namna inavyonasibiana na Yeye, kutakasika ni Kwake, bila kufananisha wala kueleza namna ulivyo.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
يَسۡـَٔلُهُۥ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ كُلَّ يَوۡمٍ هُوَ فِي شَأۡنٖ
Wanamuomba Yeye walioko mbinguni na ardhini haja zao. Hakuna yoyote anayejitosheleza kutomhitajia Yeye, kutakasika ni Kwake. Kila siku Yeye Yuko kwenye jambo: Anatukuza na Anatweza, Anatoa na Anazuia.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
سَنَفۡرُغُ لَكُمۡ أَيُّهَ ٱلثَّقَلَانِ
Nitawatengea kipindi cha kuwahesabu na kuwalipa kwa matendo yenu mliyoyafanya, enyi vizito viwili:-majini na binadamu-, tuwatese watu wa maasia na tuwape malipo mema watu wa utiifu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
يَٰمَعۡشَرَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِ إِنِ ٱسۡتَطَعۡتُمۡ أَن تَنفُذُواْ مِنۡ أَقۡطَارِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ فَٱنفُذُواْۚ لَا تَنفُذُونَ إِلَّا بِسُلۡطَٰنٖ
Enyi mkusanyiko wa majini na binadamu! Mkiweza kuihepa amri ya Mwenyezi Mungu na uamuzi Wake kwa kukimbia kwenye pambe za mbingu na ardhi basi fanyeni, na hamuwezi kufanya hivyo isipokuwa kwa nguvu na hoja na amri inayotoka kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka. (Na vipi mtaweza kufanya hivyo na hali nyinyi hamzimilikii nafsi zenu manufaa yoyote wala madhara?).
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
يُرۡسَلُ عَلَيۡكُمَا شُوَاظٞ مِّن نَّارٖ وَنُحَاسٞ فَلَا تَنتَصِرَانِ
Mtatumiwa mroromo wa moto na shaba iliyoyayushwa, mmiminiwe juu ya vichwa vyenu msiweze kusaidiana.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazukanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَإِذَا ٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ وَرۡدَةٗ كَٱلدِّهَانِ
Na pindi mbingu itakapopasuka na kuachana Siku ya Kiyama, ikawa nyekundu kama rangi ya waridi na kama mafuta yaliyochemshwa na risasi iliyoyayushwa, kutokana na mambo magumu na vituko vya Siku ya Kiyama.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُسۡـَٔلُ عَن ذَنۢبِهِۦٓ إِنسٞ وَلَا جَآنّٞ
Katika Siku hiyo Malaika hawatawauliza wale wahalifu, miongoni mwa binadamu na majini, kuhusu dhambi zao.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
يُعۡرَفُ ٱلۡمُجۡرِمُونَ بِسِيمَٰهُمۡ فَيُؤۡخَذُ بِٱلنَّوَٰصِي وَٱلۡأَقۡدَامِ
Malaika watawajua wahalifu kwa alama zao, hapo wawashike kwenye paa za vichwa vyao na nyayo zao wawarushe Motoni.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
هَٰذِهِۦ جَهَنَّمُ ٱلَّتِي يُكَذِّبُ بِهَا ٱلۡمُجۡرِمُونَ
Wataambiwa hao wahalifu kwa njia ya kulaumiwa na kudhalilishwa, «Huu ndio moto wa Jahanamu ambao wahalifu duniani walikuwa wakiukanusha:
আরবি তাফসীরসমূহ:
يَطُوفُونَ بَيۡنَهَا وَبَيۡنَ حَمِيمٍ ءَانٖ
mara wanaadhibiwa kwenye Jaḥīm, na mara nyingine wananyweshwa Hāmīm, nacho ni kinywaji kilichofikia upeo wa ukali wa moto, kinakata tumbo na sehemu za ndani ya mbavu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَلِمَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ
Na anayemcha Mwenyezi Mungu, miongoni mwa waja Wake binadamu na majini, akaogopa kusimama kwake mbele Yake, akamtii na akaacha kumuasi atakuwa na mabustani mawili ya Pepo.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
ذَوَاتَآ أَفۡنَانٖ
Mabustani mawili hayo ya Pepo yana matawi yaliyostawi kwa matunda ya kila aina.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
فِيهِمَا عَيۡنَانِ تَجۡرِيَانِ
Katika Pepo mbili hizo kuna chemchemi mbili za maji zinazopita katikati yake.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
فِيهِمَا مِن كُلِّ فَٰكِهَةٖ زَوۡجَانِ
Katika mabustani hayo mawili ya Pepo kuna sampuli mbili za kila aina ya matunda.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ فُرُشِۭ بَطَآئِنُهَا مِنۡ إِسۡتَبۡرَقٖۚ وَجَنَى ٱلۡجَنَّتَيۡنِ دَانٖ
Na wale wanaoogopa kusimama mbele ya Mola Wao watakuwa na mabustani mawili ya Pepo, ambayo ndani yake watastarehe, hali ya kutegemea juu ya matandiko yaliyojazwa dibaji nzito. Na matunda ya mabustani mawili hayo ya pepo yako karibu nao.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mtazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
فِيهِنَّ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ لَمۡ يَطۡمِثۡهُنَّ إِنسٞ قَبۡلَهُمۡ وَلَا جَآنّٞ
Katika matandiko hayo wapo wake macho yao yanawatazama waume zao tu, hawawatazami wengineo, wamefungamana na wao. Hakuna aliyewaingilia, kabla ya hao waume zao, binadamu yoyote wala jini.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadanu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
كَأَنَّهُنَّ ٱلۡيَاقُوتُ وَٱلۡمَرۡجَانُ
Kama kwamba hawa wake wa kihurulaini ni yakuti na marijani katika sifa zao na uzuri wao.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa najini na binadamu , mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
هَلۡ جَزَآءُ ٱلۡإِحۡسَٰنِ إِلَّا ٱلۡإِحۡسَٰنُ
Je atakuwa na malipo yoyote, huyu aliyekuwa mwema wa matendo duniani, isipokuwa ni afanyiwe wema kwa kupewa Pepo huko Akhera?
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ
Na chini ya mabustani ya Pepo mawili yaliyotangulia kuna mabustani ya Pepo mawili mengine.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
مُدۡهَآمَّتَانِ
Mabustani haya mawili ni rangi ya kijani. Ujani wake umeiva sana mapaka umeingia kwenye weusi.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
فِيهِمَا عَيۡنَانِ نَضَّاخَتَانِ
Ndani ya mabustani mawili hayo ya Peponi kuna chemchemi mbili zenye kububujika maji daima bila kukatika.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
فِيهِمَا فَٰكِهَةٞ وَنَخۡلٞ وَرُمَّانٞ
Kwenye mabustani hayo mawili kuna aina za matunda, mitende na mikomamanga.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
فِيهِنَّ خَيۡرَٰتٌ حِسَانٞ
Ndani ya mabustani haya manne ya Pepo kuna wake walio wema wa tabia na wazuri wa nyuso.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
حُورٞ مَّقۡصُورَٰتٞ فِي ٱلۡخِيَامِ
Mahurulaini wakunjufu wa macho, waliositiriwa na kuhifadhiwa mahemani.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
لَمۡ يَطۡمِثۡهُنَّ إِنسٞ قَبۡلَهُمۡ وَلَا جَآنّٞ
Hawajaingiliwa Mahurulaini hawa na binadamu yoyote wala jini kabla ya waume zao.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ رَفۡرَفٍ خُضۡرٖ وَعَبۡقَرِيٍّ حِسَانٖ
Hali ya kuwa wametegemea kwenye mito yenye mifuko rangi ya kijani na matandiko mazuri.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
আরবি তাফসীরসমূহ:
تَبَٰرَكَ ٱسۡمُ رَبِّكَ ذِي ٱلۡجَلَٰلِ وَٱلۡإِكۡرَامِ
Zimekithiri mno baraka za Jina la Mola wako, na kheri Zake zimekuwa nyingi, Mwenye haiba kubwa, utukufu wenye kukamilika na takrima kwa wenye kumtegemea Yeye.
আরবি তাফসীরসমূহ:
 
অর্থসমূহের অনুবাদ সূরা: সূরা আর-রাহমান
সূরাসমূহের সূচী পৃষ্ঠার নাম্বার
 
কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ - সোয়াহিলি ভাষায় অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ ও নাসির খামীস - অনুবাদসমূহের সূচী

সোয়াহিলি ভাষায় আল-কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ। ড. আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ আবূ বকর এবং শায়েখ নাসির খামীস অনূদিত।

বন্ধ