কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ - সোয়াহিলি ভাষায় অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ ও নাসির খামীস * - অনুবাদসমূহের সূচী


অর্থসমূহের অনুবাদ সূরা: সূরা আল-ফাজর   আয়াত:

Surat Al-Fajr

وَٱلۡفَجۡرِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa alfajiri
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَلَيَالٍ عَشۡرٖ
na masiku kumi ya kwanza ya Mfungotatu na kwa kile kilichoyafanya yawe matukufu,
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلشَّفۡعِ وَٱلۡوَتۡرِ
kwa kila idadi igawanyikayo na isiyogawanyika,
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَسۡرِ
kwa usiku upitapo na giza lake.
আরবি তাফসীরসমূহ:
هَلۡ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٞ لِّذِي حِجۡرٍ
Kwani hakuna katika kiapo kiliyotajwa chenye kukinaisha kwa mwenye akili?
আরবি তাফসীরসমূহ:
أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ
Huoni, ewe Mtume, vipi Mola wako
আরবি তাফসীরসমূহ:
إِرَمَ ذَاتِ ٱلۡعِمَادِ
Alivyoiangamiza kaumu ya Ād'. kabila la Irama lenye nguvu na majengo yaliyoinuliwa juu ya vipia,
আরবি তাফসীরসমূহ:
ٱلَّتِي لَمۡ يُخۡلَقۡ مِثۡلُهَا فِي ٱلۡبِلَٰدِ
ambalo hakukuumbwa mfano wake katika miji, kwa ukubwa wa miili na wingi wa nguvu?
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ
Na vipi Alivyowafanya Thamūd, kaumu ya Ṣāliḥ, ambao waliweza kuchonga jabali na kufanya nyumba ndani yake?
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَفِرۡعَوۡنَ ذِي ٱلۡأَوۡتَادِ
Na vipi Alivyomfanya Firauni, mfalme wa Misri, aliyekuwa na askari waliouhami ufalme wake na kuutilia nguvu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
ٱلَّذِينَ طَغَوۡاْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ
Hawa ndio waliokitumia nguvu na kudhulumu mijini.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَأَكۡثَرُواْ فِيهَا ٱلۡفَسَادَ
Wakaeneza humo, kwa dhuluma zao, uharibifu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَصَبَّ عَلَيۡهِمۡ رَبُّكَ سَوۡطَ عَذَابٍ
Mwenyezi Mungu Akawamiminia adhabu kali.
আরবি তাফসীরসমূহ:
إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلۡمِرۡصَادِ
Hakika Mola wako,ewe Mtume, Anamwangalia mwenye kumuasi kwa kumpa muhula kidogo, kisha Humpatiliza kwa uwezo na ushindi..
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَأَمَّا ٱلۡإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكۡرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَكۡرَمَنِ
Huyu binadamu, Mola wake Anapompa mtihani wa neema, Anapomkunjulia riziki yake na kumpa maisha mazuri, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye ana cheo kwa Mola wake na huwa akisema :»Mola wangu Amenitukuza.»
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيۡهِ رِزۡقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَهَٰنَنِ
Na Anapomuonja na Akambania riziki yake, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye amefanywa mnyonge na Mwenyezi Mungu na huwa akisema: «Mola wangu Amenifanya mnyonge.».
আরবি তাফসীরসমূহ:
كَلَّاۖ بَل لَّا تُكۡرِمُونَ ٱلۡيَتِيمَ
Hali ya mambo si kama anavyodhania binadamu huyu, kwani mtu hutukuzwa kwa kumtii Mwenyzi Mungu na hufanywa mnyonge kwa kumuasi Mwenyezi Mungu. Na nyinyi hamwakirimu mayatima na kuwatendea wema.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَلَا تَحَٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hamhimizani kulisha maskini.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَتَأۡكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكۡلٗا لَّمّٗا
Na mnakula haki za watu, katika kurithi, kwa pupa.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبّٗا جَمّٗا
Na mnapenda mali kupita kiasi.
আরবি তাফসীরসমূহ:
كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا
Basi hali zenu zisiwe namna hiyo. Kumbukeni pindi ardhi itakapotikiswa na kuvunjwavunjwa.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا
Na Akaja Mola wako kutoa uamuzi kwa waja Wake hali Malaika wamepiga safu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ
Na ukaletwa, Siku Hiyo kubwa, moto wa Jahanamu. Hiyo ndiyo Siku kafiri atakumbuka na kutubia. Kutamfalia nini sasa kukumbuka kwake na kutubia, na yeye katika ulimwengu alikuwa ameyapuuza hayo, na wakati wake umekwisha kupita?
আরবি তাফসীরসমূহ:
يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي
Atakuwa akisema: ‘Laiti mimi nilitanguliza ulimwenguni amali zenye kunifaa katika maisha yangu ya Akhera’.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ
Katika Siku Hiyo ngumu yenye vituko, hakuna atakaye kuweza kuadhibu kama adhabu ya Mwenyezi Mungu kwa anayemuasi.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ
Na hakuna atakaye kuweza kufunga kama kifungo Chake wala kufikia hadi yake.
আরবি তাফসীরসমূহ:
يَٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ
Ewe nafsi iliyotulia kwa kumtaja Mwenyezi Mungu, kumwamini Yeye na kuamini starehe ya Pepo Aliyowaandalia waumini!
আরবি তাফসীরসমূহ:
ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ
Rudi kwa Mola wako hali ya kuridhika na takrima ya Mwenyezi Mungu kwako na hali ya kuwa Mwenyezi Mungu Ameridhika na wewe.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي
Ingia miongoni mwa waja wa Mwenyezi Mungu walio wema
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي
na ingia kwenye Pepo yangu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
 
অর্থসমূহের অনুবাদ সূরা: সূরা আল-ফাজর
সূরাসমূহের সূচী পৃষ্ঠার নাম্বার
 
কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ - সোয়াহিলি ভাষায় অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ ও নাসির খামীস - অনুবাদসমূহের সূচী

সোয়াহিলি ভাষায় আল-কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ। ড. আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ আবূ বকর এবং শায়েখ নাসির খামীস অনূদিত।

বন্ধ