Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Sadržaj prijevodā


Prijevod značenja Ajet: (3) Sura: Sura el-Bekara
ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡغَيۡبِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَمِمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡ يُنفِقُونَ
Nao ndio wanao amini ghaibu (ghayb), ambayo haifikiliwi na hisia zao na akili zao pekee, kwa kuwa haijulikani isipokuwa kupitia wahyi wa Mwenyezi Mungu kwa Mtume wake, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani imshukie, kama kuamini Malaika, pepo, moto, na mengineyo katika yale yaliyoelezwa na Mtume Wake, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie yeye. Imani (Īmān) ni neno lililokusanya kumkubali Mwenyezi Mungu, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Siku ya Mwisho na Kadari (Qadar), kheri yake na shari yake. Na kutilia nguvu kukubali huko kwa maneno na vitendo, kwa moyo, ulimi na viungo. Na wao, pamoja na kuamini kwao mambo ya ghaibu yasiyoonekana, wanasimamisha Swala kwa kuchunga nyakati zake na kuzitekeleza ipasavyo kulingana na sheria ya Mwenyezi Mungu kwa Nabii wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye yeye. Kadhalika, katika kile tulichowapa wao, miongoni mwa mali, wanatoa sadaka ya mali zao ya wajibu na ya suna.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Ajet: (3) Sura: Sura el-Bekara
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Zatvaranje