Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Sadržaj prijevodā


Prijevod značenja Ajet: (3) Sura: Sura el-Maida
حُرِّمَتۡ عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَيۡتَةُ وَٱلدَّمُ وَلَحۡمُ ٱلۡخِنزِيرِ وَمَآ أُهِلَّ لِغَيۡرِ ٱللَّهِ بِهِۦ وَٱلۡمُنۡخَنِقَةُ وَٱلۡمَوۡقُوذَةُ وَٱلۡمُتَرَدِّيَةُ وَٱلنَّطِيحَةُ وَمَآ أَكَلَ ٱلسَّبُعُ إِلَّا مَا ذَكَّيۡتُمۡ وَمَا ذُبِحَ عَلَى ٱلنُّصُبِ وَأَن تَسۡتَقۡسِمُواْ بِٱلۡأَزۡلَٰمِۚ ذَٰلِكُمۡ فِسۡقٌۗ ٱلۡيَوۡمَ يَئِسَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن دِينِكُمۡ فَلَا تَخۡشَوۡهُمۡ وَٱخۡشَوۡنِۚ ٱلۡيَوۡمَ أَكۡمَلۡتُ لَكُمۡ دِينَكُمۡ وَأَتۡمَمۡتُ عَلَيۡكُمۡ نِعۡمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ ٱلۡإِسۡلَٰمَ دِينٗاۚ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ فِي مَخۡمَصَةٍ غَيۡرَ مُتَجَانِفٖ لِّإِثۡمٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Mwenyezi Mungu Amewaharamishia mfu, naye ni mnyama aliyekufa mwenyewe bila ya kuchinjwa. Na pia Amewaharamishia nyinyi damu inayotiririka inayomwagwa, nyama ya nguruwe, mnyama ambaye wakati wa kuchinjwa ametajiwa jina lisilokuwa la Mwenyezi Mungu, mnyama aliyenyongwa kwa kuzibwa pumzi zake mpaka akafa, mnyama aliyekufa kwa kupigwa gongo au jiwe, mnyama aliyeanguka kutoka mahali pa juu au aliyeanguka kisimani akafa na mnyama aliyekufa kwa kupigwa pembe na mwenzake. Na pia Amewaharamishia mnyama aliyeliwa na mnyama mwingine kama simba, chuimarara, mbwamwitu na mfano wake. Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na sifa za upungufu, Amewatoa, miongoni mwa wale Aliowaharamisha, kuanzia wale walionyongeka na waliofuatia, wale mliowahi kuwachinja kabla hawajafa, hao ni halali kwenu. Na Amewaharamishia nyinyi wanyama waliochinjiwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu miongoni mwa vitu vilivyosimamishwa viabudiwe, viwe ni mawe au vinginevyo. Na Amewaharamishia kutaka kujua mambo, mliyoandikiwa na msiyoandikiwa, kwa viapo; navyo ni vipande ambavyo walikuwa wakitaka uamuzi kwavyo wakitaka kufanya jambo kabla hawajalifanya. Hayo mliyotajiwa katika aya hii kati ya yaliyoharamishwa, yakifanywa, huwa ni kutoka kwenye amri ya Mwenyezi Mungu na twaa Yake na kwenda kwenye maasia. Sasa imekatika tamaa ya makafiri kwamba nyinyi mtaiacha Dini yenu muende kwenye ushirikina baada ya mimi kuwapa ushindi juu yao. Basi msiwaogope wao na mniogope mimi. Leo nimeshawakamilishia dini yenu, Dini ya Uislamu, kwa kuuhakikisha ushindi na kuikamilisha Sheria, nimewatimizia neema zangu kwenu kwa kuwatoa kwenye giza la ujinga na kuwapeleka kwenye mwangaza wa Imani na nimewaridhia kwamba Uislamu ndio Dini, basi shikamaneni nayo wala msiiache. Na yule aliyepatikana na dharura ya njaa ikambidi ale mfu, na akawa hakukusudia kutenda kosa, basi inafaa kwake kumla. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kumsamehe na ni Mwenye huruma naye.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Ajet: (3) Sura: Sura el-Maida
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Zatvaranje