Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Sadržaj prijevodā

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Prijevod značenja Sura: Sura el-Beled   Ajet:

Surat Al-Balad

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Naapa kwa Mji huu!
Naapa kiapo cha mkazo kwa mji wa Makka, mji mtakatifu;
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Nawe unaukaa Mji huu.
Na wewe unaishi katika mji huu, unauzidisha utukufu wake na cheo chake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
Na naapa kwa mzazi na anacho kizaa, na kwa hao wawili ndio jinsi inahifadhika na maendeleo yanabakia.
Tefsiri na arapskom jeziku:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ
Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
Hakika Sisi tumemuumba mtu katika mashaka na taabu tangu mwanzo wake mpaka kumalizika mambo yake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
Je! Anadhani mtu aliye umbwa katika mashaka haya kuwa hapana awezae kumdhalilisha?
Tefsiri na arapskom jeziku:
يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
Anasema: Nimetumia katika kupambana na Muhammad s.a.w. na kuupinga wito wake mali mengi ukiyakusanya pamoja.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
Ati anadhani kwamba mambo yake hayo yamefichikana, hayajui yeyote hata huyo aliye muumba?
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ
Kwani hatukumpa macho mawili?
Kwani Sisi hatukumuumba na macho mawili ya kutazamia,?
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ
Na ulimi, na midomo miwili?
Na ulimi na midomo miwili ili aweze kutamka na kusema sawa?
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ
Na tukambainishia zote njia mbili?
Na tukamwonyesha njia ya kheri na ya shari, na tukamtengenezea aweze kuchagua mojawapo?
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
Basi huyo hakunafiika kwa tuliyo mtengenezea, wala hakuivuka njia ya milimani inayo mzuia asifikie uwokovu, nayo ni choyo wa nafsi yake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
Na kitu gani kitakufunza nini huko kujitoma kwenye njia ya milimani?
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَكُّ رَقَبَةٍ
Kumkomboa mtumwa;
Kumkomboa mtu kutokana na utumwa,
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ
Au kumlisha siku ya njaa
Au kumlisha siku ya njaa
Tefsiri na arapskom jeziku:
يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ
Yatima aliye jamaa,
Yatima aliye jamaa wa kumliwaza kwa ujamaa na ufakiri.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ
Au masikini aliye vumbini.
Au masikini mwingi wa haja na kufakirika.
Tefsiri na arapskom jeziku:
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
Tena awe pamoja na hayo miongoni mwa wenye Imani wanao usiana na wenzao kwa subira na kuoneana huruma.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
Hao wanao sifika kwa sifa hizi, ndio watu wa kheri, wa mkono wa kulia.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
Na walio zikataa dalili tulizo zisimamisha kuthibitisha Haki kutoka na Kitabu na hoja zake, hao ndio wapotovu watu waovu walio kosa kheri na watapata adhabu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.
Juu yao utakuwa Moto ulio bebeana na milango yake ikafungwa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Sura: Sura el-Beled
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Zatvaranje