Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Sadržaj prijevodā

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Prijevod značenja Sura: Sura ed-Duha   Ajet:

Surat Ad-Duha

وَٱلضُّحَىٰ
Naapa kwa mchana!
Naapa kwa wakati wa kupanda juu jua, na ni wakati wa uchangamfu na kazi!
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku unapo tanda!
Na naapa kwa usiku unapo tulia na ukatanda kote kiza chake!
Tefsiri na arapskom jeziku:
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
Ewe Muhammad! Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukuchukia.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
Na matokeo ya mambo yako, mwisho wake, yatakuwa bora kuliko mwanzo wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
Na ninaapa kuwa bila ya shaka hapo Mola wako Mlezi atakupa kheri za duniani na Akhera hata utaridhia.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
Kwani hakukukuta wewe yatima unahitaji wa kukutunza naye akakupa makaazi ya kukuhifadhi kwa mwenye kukuangalia vyema kwa mambo yako?
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na akakukuta umepotea akakuongoa?
Na akakuona umebabaika hukukinaika na itikadi zilizo kuzunguka, naye akakuongoa kwenye Njia ya Haki?
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
Akakukuta fakiri wa mali naye akakutajirisha kwa kukupa riziki?
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimwonee!
Ikiwa hii ndiyo hali yetu nawe, basi yatima usimdhili,
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
Na mwenye kuomba au kuuliza usimjibu kwa ukavu,
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
Na ama neema za Mola wako Mlezi zitangaze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kuwa ndio kudhihirisha neema.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Sura: Sura ed-Duha
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Zatvaranje