Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Übersetzungen


Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: An-Nâzi‘ât   Vers:

Surat An-Nazi'at

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Malaika ambao huzing’oa roho za makafiri mng’oo mkali.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا
Na kwa Malaika ambao huzitukua roho za Waumini kwa uchangamfu na upole.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا
Na kwa Malaika wanaoogelea katika kushuka kwao kutoka mbinguni na kupaa kwao kwenda mbinguni.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا
Na kwa Mlaika ambao wanakimbilia kutekeleza amri za Mwenyezi Mungu.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا
Na kwa Malaika wanaopitisha amri za Mola wao katika mambo ya ulimwengu waliowakilishwa kuyafanya na kuyasimamia, - Wala haifai kwa kiumbe kukiapia chochote kile, bali yapasa kiapo chake kiwe ni kwa jina la Mola wake Muumba au sifa Zake. Na lau ataapa kwa asiye Muumba wake, basi huyo amekuwa mshirikina - Watafufuliwa viumbe bila shaka na watahesabiwa.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Siku ambayo ardhi itatetemeka kwa mvuvuo wa kwanza:
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
mvuvio wa kufisha, ukifuatiwa na mvuvio mwingine wa kuhuisha.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ
Nyoyo za makafiri, Siku hiyo, zitakuwa na papatiko kwa kicho kikubwa.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ
Macho ya makafiri hao yatakuwa madhalilifu kwa kitisho watakachokiona.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ
Wanasema hawa wakanushao kufufuliwa:
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ
«Je, tutarudishwa baada ya kufa kwetu kwenye yale tuliyokuwa nayo katika ardhi? Je, tutarudishwa na hali tushakuwa mifupa iliochakaa?»
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ
Wakasema: «Kurejea kwetu huko kutakuwa kutupu kusikokuwa kweli.’
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ
Hakika tukio hilo litakuwa kwa mvivio mmoja tu.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Wakitahamaki wao wako hai juu ya ardhi baada ya kuwa walikuwa ndani yake.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Je imekujilia, ewe Mtume, habari ya Mūsā?
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى
Pindi Mola wake Alipomwita katika bonde lililotakaswa na kubarikiwa, la Ṭuwā. Akamwambia:
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
«Enda kwa Firauni. Hakika yeye amekiuka mno katika kuasi.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Ukamwambie, ‘Je, unapendelea kuitakasa nafsi yako na upungufu na kuipamba na imani?
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ
Na nikuelekeze njia ya kumtii Mola wako, upate kumcha na kumuogopa?’»
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Mūsā alimuonyesha Firauni alama kubwa: fimbo na mkono.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
Hapo Firauni alimkanusha Nabii wa Mwenyezi Mungu , naye ni Mtume Mūsā, amani imshukie, na alimuasi Mola wake Aliyetukuka.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ
Kisha alikengeuka hali ya kuipa mgongo Imani na kufanya bidii katika kumpinga Mūsā.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
Hapo aliwakusanya raia wa utawala wake na akawaita kwa
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ
kuwaambia,»Mimi ndiye mola wenu ambaye hakuna mola mwengine aliye juu yake.»
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ
Hapo Mwenyezi Mungu Alimtesa kwa adhabu ya duniani na ya Akhera.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ
Na Akaifanya adhabu hiyo iwe ni mazingatio na ni onyo kwa watu mfano wake kati ya wale waasi. Hakika Firauni na kile kilichompata cha adhabu ni mawaidha kwa mwenye kuwaidhika na kutishika.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا
Je, kufufuliwa kwenu, enyi watu, baada ya kufa ni kugumu zaidi, katika vipimo vyenu, au ni kuumbwa kwa mbingu?
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا
Amezipanga juu yenu kama jengo. Na Ameinua sakafu yake angani, haina tofauti wala nyufa.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا
Na Ameutia giza usiku wake kwa kutwa kwa jua lake. Na Ameweka wazi mchana wake kwa kuchomoza kwake.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ
Na ardhi baada ya kuumba mbingu Ameitandaza. Na Ameweka humo manufaa yake.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا
Na Ametumbua humo chemchemu za maji. Na Ameotesha humo mimea inayolishwa.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا
Na Ameyakita humo majabali yakiwa ni vigingi vyake. Ameumba, Aliyetakasika na kila upungufu,
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
neema zote hizi zikiwa ni manufaa kwenu na kwa wanyama wenu. (Hakika kurudisha kuumbwa kwenu, Siku ya Kiyama, ni sahali kwa Mwenyezi Mungu kushinda kuumba viumbe hivyo vyingine. Na vyote hivyo, kwa Mwenyezi Mungu, ni rahisi na ni vipesi).
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Pindi kitakapokuja Kiyama Kikubwa na balaa nzito, nao ni Mvuvio wa pili. Kipindi hicho zitaoneshwa kwa binadamu vitendo vyake vyote, za kheri na za shari.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ
Hapo atazikumbuka na kuzitambua.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
Na utaoneshwa Moto wa Jahanamu kwa kila aonaye, uwe waonekana waziwazi.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
Ama yule atakayekiuka amri ya Mwenyezi Mungu
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
na akapendelea maisha ya ulimwenguni kuliko ya Akhera,
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
basi kwa kweli marejeo yake ni Motoni.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ
Na ama yule atakayeogopa kusimama mbele ya Mwenyezi Mungu kuhesabiwa na akaikanya nafsi yake na matamanio mapotofu,
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
basi Peponi ndiko makazi yake.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا
Wanakuuliza washirikina, ewe Mtume, kwa madharau, kuhusu wakati wa kuanzia Kiyama unachowaonya.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ
Wewe huna kamwe ujuzi nacho.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Bali mambo ya ujuzi huo yarejeshwe kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye Sifa Tukufu.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا
Wewe linalokuhusu katika habari zake ni kumuonya nacho yule anayekiogopa.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا
Kama kwamba wao siku watakapouona Kiyama kimesimama, watakuwa hawakukaa katika maisha yao ya duniani, kwa vituko vya hiko Kiyama, isipokuwa ni kama kwamba wamkaa kati ya adhuhuri mpaka kutwa juwa, au ni kama kati ya kuchomoza jua mpaka nusu ya mchana.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: An-Nâzi‘ât
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Übersetzungen

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Schließen