Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Übersetzungen


Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: Al-Bayyinah   Vers:

Surat Al-Bayyinah

لَمۡ يَكُنِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ مُنفَكِّينَ حَتَّىٰ تَأۡتِيَهُمُ ٱلۡبَيِّنَةُ
Hawakuwa wenye kukufuru miongoni mwa Mayhudi na Wanaswara na washirikina ni wenye kuacha ukafiri wao mpaka uwajilie wao ushahidi walioahidiwa katika vitabu vilivyopita.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
رَسُولٞ مِّنَ ٱللَّهِ يَتۡلُواْ صُحُفٗا مُّطَهَّرَةٗ
Nao ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, atakayewasomea Qur’ani iliyomo kwenye kurasa safi.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فِيهَا كُتُبٞ قَيِّمَةٞ
Ndani ya kurasa hizo mna habari za kweli na amri za uadilifu zenye kuongoza kwenye haki na kwenye njia ilionyoka.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَمَا تَفَرَّقَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُمُ ٱلۡبَيِّنَةُ
Na hawakutofautiana wale waliopewa Kitabu, miongoni mwa Mayahudi na Wanaswara, juu ya kuwa Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ni Mtume wa kweli, kwa sifa zake waliokuwa wakiziona katika vtabu vyao isipokuwa baada ya kuwathibitikia kuwa yeye ndiye Nabii waliyoahidiwa katika Taurati na Injili. Walikuwa wanakubali , kwa umoja wao, kuwa unabii wake ni wa kweli. Lakini alipotumilizwa waliukanusha na wakatofautiana.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَمَآ أُمِرُوٓاْ إِلَّا لِيَعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَ حُنَفَآءَ وَيُقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَيُؤۡتُواْ ٱلزَّكَوٰةَۚ وَذَٰلِكَ دِينُ ٱلۡقَيِّمَةِ
Na hawakuamrishwa katika sheria zote zilizopita isipokuwa ni wamuabudu Mwenyezi Mungu Peke Yake, wakikusudia kwa ibada yao kupata Radhi Zake, hali ya kuepuka upande wa ushirikina na kuelekea kwenye Imani, wasimamishe Swala na watoe Zaka. Kufanya hayo ndio Dini iliyolingana , nayo ni Uislamu.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَآۚ أُوْلَٰٓئِكَ هُمۡ شَرُّ ٱلۡبَرِيَّةِ
Hakika wale waliokufuru miongoni mwa Mayahudi na Wanaswara na Washirikina, mateso yao ni Moto wa Jahanamu. Watakuwa ni wenye kukaa milele humo. Wao ndio viumbe waovu kabisa.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ أُوْلَٰٓئِكَ هُمۡ خَيۡرُ ٱلۡبَرِيَّةِ
Hakika wale waliomuamini Mwenyezi Mungu, wakamfuata Mtume wake na wakafanya amali njema, wao ndio bora wa viumbe.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
جَزَآؤُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّٰتُ عَدۡنٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ رَّضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُۚ ذَٰلِكَ لِمَنۡ خَشِيَ رَبَّهُۥ
Malipo yao , mbele ya Mola wao Siku ya Kiyama, ni Pepo ya makazi na utulivu yenye upeo wa uzuri, ambayo chini ya majumba yake ya fahari inapita mito; watakaa milele humo. Mwenyezi Mungu Ameridhika nao Akakubali amali zao njema. Na wao wameridhika na Yeye kwa maandalio Aliyowafanyia ya aina mbalimbali za takrima. Malipo mazuri hayo ni ya aliyemuogopa Mweyezi Mungu na akajiepusha na maasia.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: Al-Bayyinah
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Übersetzungen

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Schließen