Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman * - Translations’ Index


Translation of the meanings Ayah: (7) Surah: Al-Hujurāt
وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ فِيكُمۡ رَسُولَ ٱللَّهِۚ لَوۡ يُطِيعُكُمۡ فِي كَثِيرٖ مِّنَ ٱلۡأَمۡرِ لَعَنِتُّمۡ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ حَبَّبَ إِلَيۡكُمُ ٱلۡإِيمَٰنَ وَزَيَّنَهُۥ فِي قُلُوبِكُمۡ وَكَرَّهَ إِلَيۡكُمُ ٱلۡكُفۡرَ وَٱلۡفُسُوقَ وَٱلۡعِصۡيَانَۚ أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلرَّٰشِدُونَ
Na mjue kuwa baina yenu yupo Mtume wa Mwenyezi Mungu, kuweni na adabu na yeye, kwani yeye anayajua zaidi mambo yanayowafaa kuliko nyinyi, anawatakia nyinyi kheri, na nyinyi huenda mkajitakia shari na madhara ambayo Mtume hawakubalii, na lau yeye angaliwafuata nyinyi katika mengi mnayoyachagua, hilo lingalipelekea muingie kwenye usumbufu. Lakini Mwenyezi Mungu Amewafanya nyinyi muipende Imani na Akaifanya ipambike ndani ya nyoyo zenu ndipo mkaamini, na Amewafanya nyinyi mchukie kumkanusha Mwenyezi Mungu, kutoka nje ya twaa Yake na kumuasi. Hao waliosifika kwa sifa hizi ndio waongofu wenye kufuata njia ya haki.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (7) Surah: Al-Hujurāt
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

close