Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany * - Translations’ Index

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Translation of the meanings Ayah: (14) Surah: Ash-Shūra
وَمَا تَفَرَّقُوٓاْ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَهُمُ ٱلۡعِلۡمُ بَغۡيَۢا بَيۡنَهُمۡۚ وَلَوۡلَا كَلِمَةٞ سَبَقَتۡ مِن رَّبِّكَ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗى لَّقُضِيَ بَيۡنَهُمۡۚ وَإِنَّ ٱلَّذِينَ أُورِثُواْ ٱلۡكِتَٰبَ مِنۢ بَعۡدِهِمۡ لَفِي شَكّٖ مِّنۡهُ مُرِيبٖ
Na hawakufarikiana ila baada ya kuwajia ilimu kwa sababu ya husuda iliyo kuwa baina yao. Na lau kuwa haikwisha tangulia kauli kutoka kwa Mola wako Mlezi ya kuakhirisha mpaka muda maalumu, basi bila ya shaka palingeli hukumiwa baina yao. Na hakika walio rithishwa Kitabu baada yao wanakitilia shaka inayo wahangaisha.
Wala hawakukhitalifiana katika Dini wafuasi wa Mitume walio tangulia ila baada ya kuwafikia ujuzi wa kweli, na hayo ni kwa kutokana na uadui na uhasidi ulio baina yao. Na lau kuwa si ahadi iliyo kwisha tangulia kutoka kwa Mwenyezi Mungu ya kuakhirisha adhabu mpaka Siku ya Kiyama, basi bila ya shaka walingeli teketezwa. Na kwa hakika wale walio rithishwa Kitabu kutokana na walio kabla yao, na wakawahi zama zako, wana shaka na Kitabu chao, tena shaka ya kuwatatanisha. Ndio maana hawaitikii wito wako. (Lau kuwa Mayahudi wameamini kweli yaliyomo katika Taurati, wangeli muamini Nabii Isa na Nabii Muhammad. Na lau kuwa Wakristo wameamini kweli yaliomo katika Taurati na Injili basi hapana la kuwazuia wasimuamini Nabii Muhammad, na kumuamini Mwenyezi Mungu Mmoja, wala hana Utatu. Lakini hawana imani ya yakini, na kwa hivyo wameunda mawazo yaliyo nje ya Taurati na nje ya Injili.)
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Ayah: (14) Surah: Ash-Shūra
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Ali Muhsen Alberwany - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Ali Muhsen Alberwany

close