Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis * - Índice de traducciones


Traducción de significados Capítulo: Sura An-Naazi'aat   Versículo:

Surat An-Nazi'at

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Malaika ambao huzing’oa roho za makafiri mng’oo mkali.
Las Exégesis Árabes:
وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا
Na kwa Malaika ambao huzitukua roho za Waumini kwa uchangamfu na upole.
Las Exégesis Árabes:
وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا
Na kwa Malaika wanaoogelea katika kushuka kwao kutoka mbinguni na kupaa kwao kwenda mbinguni.
Las Exégesis Árabes:
فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا
Na kwa Mlaika ambao wanakimbilia kutekeleza amri za Mwenyezi Mungu.
Las Exégesis Árabes:
فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا
Na kwa Malaika wanaopitisha amri za Mola wao katika mambo ya ulimwengu waliowakilishwa kuyafanya na kuyasimamia, - Wala haifai kwa kiumbe kukiapia chochote kile, bali yapasa kiapo chake kiwe ni kwa jina la Mola wake Muumba au sifa Zake. Na lau ataapa kwa asiye Muumba wake, basi huyo amekuwa mshirikina - Watafufuliwa viumbe bila shaka na watahesabiwa.
Las Exégesis Árabes:
يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Siku ambayo ardhi itatetemeka kwa mvuvuo wa kwanza:
Las Exégesis Árabes:
تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
mvuvio wa kufisha, ukifuatiwa na mvuvio mwingine wa kuhuisha.
Las Exégesis Árabes:
قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ
Nyoyo za makafiri, Siku hiyo, zitakuwa na papatiko kwa kicho kikubwa.
Las Exégesis Árabes:
أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ
Macho ya makafiri hao yatakuwa madhalilifu kwa kitisho watakachokiona.
Las Exégesis Árabes:
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ
Wanasema hawa wakanushao kufufuliwa:
Las Exégesis Árabes:
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ
«Je, tutarudishwa baada ya kufa kwetu kwenye yale tuliyokuwa nayo katika ardhi? Je, tutarudishwa na hali tushakuwa mifupa iliochakaa?»
Las Exégesis Árabes:
قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ
Wakasema: «Kurejea kwetu huko kutakuwa kutupu kusikokuwa kweli.’
Las Exégesis Árabes:
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ
Hakika tukio hilo litakuwa kwa mvivio mmoja tu.
Las Exégesis Árabes:
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Wakitahamaki wao wako hai juu ya ardhi baada ya kuwa walikuwa ndani yake.
Las Exégesis Árabes:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Je imekujilia, ewe Mtume, habari ya Mūsā?
Las Exégesis Árabes:
إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى
Pindi Mola wake Alipomwita katika bonde lililotakaswa na kubarikiwa, la Ṭuwā. Akamwambia:
Las Exégesis Árabes:
ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
«Enda kwa Firauni. Hakika yeye amekiuka mno katika kuasi.
Las Exégesis Árabes:
فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Ukamwambie, ‘Je, unapendelea kuitakasa nafsi yako na upungufu na kuipamba na imani?
Las Exégesis Árabes:
وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ
Na nikuelekeze njia ya kumtii Mola wako, upate kumcha na kumuogopa?’»
Las Exégesis Árabes:
فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Mūsā alimuonyesha Firauni alama kubwa: fimbo na mkono.
Las Exégesis Árabes:
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
Hapo Firauni alimkanusha Nabii wa Mwenyezi Mungu , naye ni Mtume Mūsā, amani imshukie, na alimuasi Mola wake Aliyetukuka.
Las Exégesis Árabes:
ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ
Kisha alikengeuka hali ya kuipa mgongo Imani na kufanya bidii katika kumpinga Mūsā.
Las Exégesis Árabes:
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
Hapo aliwakusanya raia wa utawala wake na akawaita kwa
Las Exégesis Árabes:
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ
kuwaambia,»Mimi ndiye mola wenu ambaye hakuna mola mwengine aliye juu yake.»
Las Exégesis Árabes:
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ
Hapo Mwenyezi Mungu Alimtesa kwa adhabu ya duniani na ya Akhera.
Las Exégesis Árabes:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ
Na Akaifanya adhabu hiyo iwe ni mazingatio na ni onyo kwa watu mfano wake kati ya wale waasi. Hakika Firauni na kile kilichompata cha adhabu ni mawaidha kwa mwenye kuwaidhika na kutishika.
Las Exégesis Árabes:
ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا
Je, kufufuliwa kwenu, enyi watu, baada ya kufa ni kugumu zaidi, katika vipimo vyenu, au ni kuumbwa kwa mbingu?
Las Exégesis Árabes:
رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا
Amezipanga juu yenu kama jengo. Na Ameinua sakafu yake angani, haina tofauti wala nyufa.
Las Exégesis Árabes:
وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا
Na Ameutia giza usiku wake kwa kutwa kwa jua lake. Na Ameweka wazi mchana wake kwa kuchomoza kwake.
Las Exégesis Árabes:
وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ
Na ardhi baada ya kuumba mbingu Ameitandaza. Na Ameweka humo manufaa yake.
Las Exégesis Árabes:
أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا
Na Ametumbua humo chemchemu za maji. Na Ameotesha humo mimea inayolishwa.
Las Exégesis Árabes:
وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا
Na Ameyakita humo majabali yakiwa ni vigingi vyake. Ameumba, Aliyetakasika na kila upungufu,
Las Exégesis Árabes:
مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
neema zote hizi zikiwa ni manufaa kwenu na kwa wanyama wenu. (Hakika kurudisha kuumbwa kwenu, Siku ya Kiyama, ni sahali kwa Mwenyezi Mungu kushinda kuumba viumbe hivyo vyingine. Na vyote hivyo, kwa Mwenyezi Mungu, ni rahisi na ni vipesi).
Las Exégesis Árabes:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Pindi kitakapokuja Kiyama Kikubwa na balaa nzito, nao ni Mvuvio wa pili. Kipindi hicho zitaoneshwa kwa binadamu vitendo vyake vyote, za kheri na za shari.
Las Exégesis Árabes:
يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ
Hapo atazikumbuka na kuzitambua.
Las Exégesis Árabes:
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
Na utaoneshwa Moto wa Jahanamu kwa kila aonaye, uwe waonekana waziwazi.
Las Exégesis Árabes:
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
Ama yule atakayekiuka amri ya Mwenyezi Mungu
Las Exégesis Árabes:
وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
na akapendelea maisha ya ulimwenguni kuliko ya Akhera,
Las Exégesis Árabes:
فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
basi kwa kweli marejeo yake ni Motoni.
Las Exégesis Árabes:
وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ
Na ama yule atakayeogopa kusimama mbele ya Mwenyezi Mungu kuhesabiwa na akaikanya nafsi yake na matamanio mapotofu,
Las Exégesis Árabes:
فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
basi Peponi ndiko makazi yake.
Las Exégesis Árabes:
يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا
Wanakuuliza washirikina, ewe Mtume, kwa madharau, kuhusu wakati wa kuanzia Kiyama unachowaonya.
Las Exégesis Árabes:
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ
Wewe huna kamwe ujuzi nacho.
Las Exégesis Árabes:
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Bali mambo ya ujuzi huo yarejeshwe kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye Sifa Tukufu.
Las Exégesis Árabes:
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا
Wewe linalokuhusu katika habari zake ni kumuonya nacho yule anayekiogopa.
Las Exégesis Árabes:
كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا
Kama kwamba wao siku watakapouona Kiyama kimesimama, watakuwa hawakukaa katika maisha yao ya duniani, kwa vituko vya hiko Kiyama, isipokuwa ni kama kwamba wamkaa kati ya adhuhuri mpaka kutwa juwa, au ni kama kati ya kuchomoza jua mpaka nusu ya mchana.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Capítulo: Sura An-Naazi'aat
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por el Dr. Abdalla Mohamed Abubakar y Nassor Khamis

Cerrar