Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis * - Índice de traducciones


Traducción de significados Capítulo: Sura Al-Burooj   Versículo:

Surat Al-Buruj

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡبُرُوجِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu zenye njia za kupitia jua na mwezi.
Las Exégesis Árabes:
وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡمَوۡعُودِ
Na kwa Siku ya Kiyama ambayo Amewaahidi viumbe kuwa Atawakusanya.
Las Exégesis Árabes:
وَشَاهِدٖ وَمَشۡهُودٖ
Na kwa shahidi, mwenye kutoa ushahidi, na mwenye kutolewa ushahidi juu yake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Anachokitaka. Lakini kiumbe hafai kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Las Exégesis Árabes:
قُتِلَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأُخۡدُودِ
Wamelaaniwa waliofukua chini ya ardhi shimo kubwa ili kuwatesa Waumini.
Las Exégesis Árabes:
ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلۡوَقُودِ
Wakawasha moto mkubwa wenye kuni nyingi.
Las Exégesis Árabes:
إِذۡ هُمۡ عَلَيۡهَا قُعُودٞ
Wakawa wamekaa kwenye kingo za shimo hilo.
Las Exégesis Árabes:
وَهُمۡ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ شُهُودٞ
Wakishuhudia vitendo vya mateso na adhabu wanavyowafanyia Waumini.
Las Exégesis Árabes:
وَمَا نَقَمُواْ مِنۡهُمۡ إِلَّآ أَن يُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ
Na hawakuwatesa mateso hayo isipokuwa wenye kuteswa walikuwa wanamuamini Mwenyezi Mungu Mshindi Asiyeshindwa, Mhimidiwa wa maneno Yake vitendo Vyake na sifa Zake.
Las Exégesis Árabes:
ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ
Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi Ambaye, kutakasika na sifa za upungufu ni kwake, Anashuhudia kila kitu, hakuna kinachofichika kwake.
Las Exégesis Árabes:
إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ
Hakika, wale waliowachoma kwa moto Waumini, wa kike na wa kiume, ili kuwazuia watu na dini ya Mwenyezi Mungu, kisha wasitubie, watapata, Siku ya Akhera, adhabu ya Jahanamu na watapata adhabu kali yenye kuchoma.
Las Exégesis Árabes:
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ
Wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya amali njema, watapata Pepo ambayo chini ya majumba yake ya kifahari yapita mito. Huko ni kufaulu kukubwa.
Las Exégesis Árabes:
إِنَّ بَطۡشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ
Hakika malipizo ya Mola wako kwa maadui Zake na mateso Yake juu yao ni mazito.
Las Exégesis Árabes:
إِنَّهُۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ
Ndiye Yeye Mwenye kuanzisha kuumba na kisha kurudisha.
Las Exégesis Árabes:
وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ
Ndiye Yeye Mwingi wa kusamehe kwa wenye kutubia, Mwingi wa mapenzi kwa wanaoikurubisha kwake.
Las Exégesis Árabes:
ذُو ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡمَجِيدُ
Mwenye Arshi tukufu.
Las Exégesis Árabes:
فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ
Mfanya Alitakalo: hakuna kitu Anachotaka kiwe kisiwe.
Las Exégesis Árabes:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡجُنُودِ
Je, ewe Mtume, imekufikia habari ya makundi yaliyokufuru na kukanusha Mitume walioletwa, ya
Las Exégesis Árabes:
فِرۡعَوۡنَ وَثَمُودَ
Firauni na Thamūd, misiba na adhabu iliyowashukia? Hawakuzingatia kwa habari hiyo.
Las Exégesis Árabes:
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي تَكۡذِيبٖ
Bali waliokufuru waendelea kukanusha kwao, kama walivyokuwa waliokuja kabla yao.
Las Exégesis Árabes:
وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطُۢ
Na Mwenyezi Mungu Amewazunguka kwa Ujuzi na Uweza Wake, hakuna chenye kufichika Kwake kuhusu wao na vitendo vyao. Hii Qu’ani siyo kama wanavyodai wenye kukanusha katika washirikina kuwa ni mashairi na uchawi ndipo wakaikanusha.
Las Exégesis Árabes:
بَلۡ هُوَ قُرۡءَانٞ مَّجِيدٞ
Bali hii ni Qur’ani kubwa iliyo tukufu,
Las Exégesis Árabes:
فِي لَوۡحٖ مَّحۡفُوظِۭ
iliyomo kwenye Ubao Uliohifadhiwa, haufikiwi na kubadilishwa wala kupotoshwa.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Capítulo: Sura Al-Burooj
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por el Dr. Abdalla Mohamed Abubakar y Nassor Khamis

Cerrar