Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany * - Índice de traducciones

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traducción de significados Capítulo: Sura Al-Fil   Versículo:

Surat Al-Fil

أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصۡحَٰبِ ٱلۡفِيلِ
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo?
Hakika, ewe Muhammad, unajua kwa ujuzi usio ingiliwa na shaka yoyote, alivyo fanya Mola wako Mlezi kuwafanyia wale watu wenye tembo (ndovu), wakataka kuishambulia Nyumba takatifu ya Al-Kaaba.
Las Exégesis Árabes:
أَلَمۡ يَجۡعَلۡ كَيۡدَهُمۡ فِي تَضۡلِيلٖ
Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?
Unajua ya kwamba hakika Mwenyezi Mungu amejaalia juhudi yao kutaka kuibomoa Al-Kaaba ivize na ipotelee mbali. Juhudi yao ikapeperuka, na wao wasipate makusudio yao.
Las Exégesis Árabes:
وَأَرۡسَلَ عَلَيۡهِمۡ طَيۡرًا أَبَابِيلَ
Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,
Na Mwenyezi Mungu aliwasalitisha na majeshi ya ndege yaliyo watokea makundi kwa makundi yakifuatana, na yakawazunguka kila upande.
Las Exégesis Árabes:
تَرۡمِيهِم بِحِجَارَةٖ مِّن سِجِّيلٖ
Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,
Wakiwatupia mawe kutoka Jahannamu.
Las Exégesis Árabes:
فَجَعَلَهُمۡ كَعَصۡفٖ مَّأۡكُولِۭ
Akawafanya kama majani yaliyo liwa!
Akawafanya kama majani ya mimea yaliyo sibiwa yakatilifu.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Capítulo: Sura Al-Fil
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por Ali Muhsen Alberwany

Cerrar