Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany * - Índice de traducciones

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traducción de significados Capítulo: Sura Ash-Sharh   Versículo:

Surat Ash-Sharh

أَلَمۡ نَشۡرَحۡ لَكَ صَدۡرَكَ
Hatukukunjulia kifua chako?
Hakika tumekukunjulia kifua chako kwa kuwa tulitia ndani yake Uwongofu na Imani.
Las Exégesis Árabes:
وَوَضَعۡنَا عَنكَ وِزۡرَكَ
Na tukakuondolea mzigo wako!
Na tumekupunguzia mizigo iliyo kuwa mizito juu ya mgongo wako, kwa kukuunga mkono na kukusahilishia mambo yako,
Las Exégesis Árabes:
ٱلَّذِيٓ أَنقَضَ ظَهۡرَكَ
Ulio vunja mgongo wako?
Ambayo yalikuwa ni mazito juu ya mgongo wako.
Las Exégesis Árabes:
وَرَفَعۡنَا لَكَ ذِكۡرَكَ
Na tukakunyanyulia utajo wako?
Na tumelitukuza jina lako, tukalifanya linatajwa na ulimi wa kila Muumini pamoja na jina letu.
Las Exégesis Árabes:
فَإِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرًا
Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi!
Hizo ni baadhi ya neema zetu juu yako. Basi kuwa na yakini na uweza wa Mwenyezi Mtukufu, kwani pamoja na uzito upo wepesi mwingi unao kuja nao.
Las Exégesis Árabes:
إِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرٗا
Hakika pamoja na uzito upo wepesi.
Hakika pamoja na uzito (wakati huo huo ijapo kuwa wewe hujui), upo wepesi mwingi vile vile.
Las Exégesis Árabes:
فَإِذَا فَرَغۡتَ فَٱنصَبۡ
Na ukipata faragha, fanya juhudi.
Basi ukipata nafasi katika kazi ya kuwalingania watu, na mambo yaliyo khusiana na Jihadi, endelea na jitihada ya ibada na jishughulishe nafsi yako katika hayo.
Las Exégesis Árabes:
وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَٱرۡغَب
Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.
Kwa Mola wako Mlezi tu ndio uelekee kwa kumwomba na kumhitajia.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Capítulo: Sura Ash-Sharh
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por Ali Muhsen Alberwany

Cerrar