Check out the new design

ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه‌ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس * - لیست ترجمه ها


ترجمهٔ معانی سوره: مسد   آیه:

Al-Masad

تَبَّتۡ يَدَآ أَبِي لَهَبٖ وَتَبَّ
Imehasirika mikono miwili ya Abu Lahab, na yeye mwenyewe ameangamia, kwa kumuudhi Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie. Hasara ya Abu Lahab ilithubutu.
تفسیرهای عربی:
مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ
Hayakumfalia kitu mali yake na watoto wake. Kwani hivyo havitamkinga na adhabu ya Mwenyezi Mungu pindi ikimshukia.
تفسیرهای عربی:
سَيَصۡلَىٰ نَارٗا ذَاتَ لَهَبٖ
Ataingia kwenye Moto wenye kuroroma,
تفسیرهای عربی:
وَٱمۡرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ
yeye na mke wake ambaye alikuwa akibeba miba na kuiweka kwenye njia anayopita Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ili kumuudhi.
تفسیرهای عربی:
فِي جِيدِهَا حَبۡلٞ مِّن مَّسَدِۭ
Kwenye shingo yake patakuwa na kamba imara ya lifu gumu lilio kavu; atabebewa nayo kwenye Moto wa Jahanamu, kisha atarushwa nayo mpaka chini.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی سوره: مسد
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه‌ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس - لیست ترجمه ها

مترجم: دکتر عبد الله محمد ابو بکر و شیخ ناصر خميس.

بستن