ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس * - لیست ترجمه ها


ترجمهٔ معانی سوره: سوره ضحى   آیه:

Surat Ad-Duha

وَٱلضُّحَىٰ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa dhuha, na uliokusudiwa ni wakati wa mchana mzima.
تفسیرهای عربی:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku utuliapo na viumbe na likashadidi giza lake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Atakacho katika viumbe vyake. Ama kiumbe, hafai kuapa kwa asiyekuwa Muumba wake. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
تفسیرهای عربی:
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Hakukuwacha Mola wako, ewe Mtume, wala Hakukuchukia kwa kuchelewesha kukuteremshiaWahyi.
تفسیرهای عربی:
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na Nyumba ya Akhera ni bora kwako kuliko nyumba ya ulimwengu.
تفسیرهای عربی:
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Atakupa Mola wako, ewe Mtume, neema ya kila sampuli uridhike.
تفسیرهای عربی:
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani Hakukupata, kabla ya hapo, kuwa ni yatima Akakukusanya na kukutunza.
تفسیرهای عربی:
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na Akakupata hujui Kitabu wala Imani, Akakufundisha yale amabayo ulikuwa huyajui na akakuafikia kufanya amali bora?
تفسیرهای عربی:
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Na Akakupata masikini, Akakuletea riziki yako na Akakutajirisha kwa kutosheka na kusubiri?
تفسیرهای عربی:
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimtende ubaya.
تفسیرهای عربی:
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na muombaji usimkaripie, bali mlishe na umtimizie haja yake.
تفسیرهای عربی:
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na ama neema ya Mola wako Aliyokuneemesha nayo izungumze.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی سوره: سوره ضحى
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی. ترجمهٔ دکتر عبدالله محمد ابوبکر و شیخ ناصر خمیس.

بستن