ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی * - لیست ترجمه ها

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

ترجمهٔ معانی سوره: سوره ضحى   آیه:

Surat Ad-Duha

وَٱلضُّحَىٰ
Naapa kwa mchana!
Naapa kwa wakati wa kupanda juu jua, na ni wakati wa uchangamfu na kazi!
تفسیرهای عربی:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku unapo tanda!
Na naapa kwa usiku unapo tulia na ukatanda kote kiza chake!
تفسیرهای عربی:
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
Ewe Muhammad! Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukuchukia.
تفسیرهای عربی:
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
Na matokeo ya mambo yako, mwisho wake, yatakuwa bora kuliko mwanzo wake.
تفسیرهای عربی:
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
Na ninaapa kuwa bila ya shaka hapo Mola wako Mlezi atakupa kheri za duniani na Akhera hata utaridhia.
تفسیرهای عربی:
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
Kwani hakukukuta wewe yatima unahitaji wa kukutunza naye akakupa makaazi ya kukuhifadhi kwa mwenye kukuangalia vyema kwa mambo yako?
تفسیرهای عربی:
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na akakukuta umepotea akakuongoa?
Na akakuona umebabaika hukukinaika na itikadi zilizo kuzunguka, naye akakuongoa kwenye Njia ya Haki?
تفسیرهای عربی:
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
Akakukuta fakiri wa mali naye akakutajirisha kwa kukupa riziki?
تفسیرهای عربی:
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimwonee!
Ikiwa hii ndiyo hali yetu nawe, basi yatima usimdhili,
تفسیرهای عربی:
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
Na mwenye kuomba au kuuliza usimjibu kwa ukavu,
تفسیرهای عربی:
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
Na ama neema za Mola wako Mlezi zitangaze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kuwa ndio kudhihirisha neema.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی سوره: سوره ضحى
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی ـ ترجمهٔ علی محسن البروانی.

بستن