Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Simoore: Simoore yerɓaango   Aaya:

Surat Az-Zalzalah

إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا
Itakapotikiswa ardhi mtikiso wa nguvu.
Faccirooji aarabeeji:
وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا
Na ikatoa vilivyomo ndani yake: wafu na makandi.
Faccirooji aarabeeji:
وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا
Na akauliza binadamu, kwa babaiko, «Imezukiwa na nini?»
Faccirooji aarabeeji:
يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا
Siku ya Kiyama ardhi itatoa habari ya mambo iliyofanyiwa ya uzuri na ubaya.
Faccirooji aarabeeji:
بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا
kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Ameiamuru itoe habari ya mambo iliyofanyiwa.
Faccirooji aarabeeji:
يَوۡمَئِذٖ يَصۡدُرُ ٱلنَّاسُ أَشۡتَاتٗا لِّيُرَوۡاْ أَعۡمَٰلَهُمۡ
Siku hiyo wataondoka kutoka kwenye kisimamo cha Hesabu wakiwa makundi, ili Mwenyezi Mungu Awaoneshe waliyoyatenda, mazuri na mabaya, na Awalipe kwayo.
Faccirooji aarabeeji:
فَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٍ خَيۡرٗا يَرَهُۥ
Yoyote mwenye kufanya jema wezani wa chungu mdogo atayaona malipo yake Akhera.
Faccirooji aarabeeji:
وَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ شَرّٗا يَرَهُۥ
Na yoyote mwenye kufanya baya wezani wa chungu mdogo atayaona malipo yake Akhera.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Simoore: Simoore yerɓaango
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawaahili, firi ɗum ko Doktoor Abdullaay Muhammad Abuubakri. E mawɗo Naasir Kamiis.

Uddude