Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo saawaahiliiwo - Ali Muhsin Al-barwaany * - Tippudi firooji ɗii

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Firo maanaaji Simoore: Simlore ñiiwo (al-fiil)   Aaya:

Surat Al-Fil

أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصۡحَٰبِ ٱلۡفِيلِ
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo?
Hakika, ewe Muhammad, unajua kwa ujuzi usio ingiliwa na shaka yoyote, alivyo fanya Mola wako Mlezi kuwafanyia wale watu wenye tembo (ndovu), wakataka kuishambulia Nyumba takatifu ya Al-Kaaba.
Faccirooji aarabeeji:
أَلَمۡ يَجۡعَلۡ كَيۡدَهُمۡ فِي تَضۡلِيلٖ
Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?
Unajua ya kwamba hakika Mwenyezi Mungu amejaalia juhudi yao kutaka kuibomoa Al-Kaaba ivize na ipotelee mbali. Juhudi yao ikapeperuka, na wao wasipate makusudio yao.
Faccirooji aarabeeji:
وَأَرۡسَلَ عَلَيۡهِمۡ طَيۡرًا أَبَابِيلَ
Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,
Na Mwenyezi Mungu aliwasalitisha na majeshi ya ndege yaliyo watokea makundi kwa makundi yakifuatana, na yakawazunguka kila upande.
Faccirooji aarabeeji:
تَرۡمِيهِم بِحِجَارَةٖ مِّن سِجِّيلٖ
Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,
Wakiwatupia mawe kutoka Jahannamu.
Faccirooji aarabeeji:
فَجَعَلَهُمۡ كَعَصۡفٖ مَّأۡكُولِۭ
Akawafanya kama majani yaliyo liwa!
Akawafanya kama majani ya mimea yaliyo sibiwa yakatilifu.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Simoore: Simlore ñiiwo (al-fiil)
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo saawaahiliiwo - Ali Muhsin Al-barwaany - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawahili, firi ɗum ko Ali Muhsin Al-barwani

Uddude