Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo saawaahiliiwo - Ali Muhsin Al-barwaany * - Tippudi firooji ɗii

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Firo maanaaji Simoore: Simoore heefereeɓe   Aaya:

Surat Al-Kafirun

قُلۡ يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡكَٰفِرُونَ
Sema: Enyi makafiri!
Ewe Muhammad! Sema: Enyi makafiri, mlio shikilia juu ya ukafiri wenu.
Faccirooji aarabeeji:
لَآ أَعۡبُدُ مَا تَعۡبُدُونَ
Siabudu mnacho kiabudu;
Mimi simuabudu mnaye muabudu nyinyi badala ya Mwenyezi Mungu.
Faccirooji aarabeeji:
وَلَآ أَنتُمۡ عَٰبِدُونَ مَآ أَعۡبُدُ
Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.
Wala nyinyi si wenye kumuabudu huyo ambaye mimi namuabudu, naye ni Mwenyezi Mungu wa pekee.
Faccirooji aarabeeji:
وَلَآ أَنَا۠ عَابِدٞ مَّا عَبَدتُّمۡ
Wala sitaabudu mnacho abudu.
Wala mimi si mwenye kuabudu mfano wa ibada yenu, kwani nyinyi ni washirikina.
Faccirooji aarabeeji:
وَلَآ أَنتُمۡ عَٰبِدُونَ مَآ أَعۡبُدُ
Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.
Wala nyinyi si wenye kuabudu mfano wa ibada yangu, kwani hii ni Tawhidi, ibada ya Mungu Mmoja.
Faccirooji aarabeeji:
لَكُمۡ دِينُكُمۡ وَلِيَ دِينِ
Nyinyi mna dini yenu, nami nina Dini yangu.
Nyinyi mna dini yenu mnayo itakidi, na mimi nina Dini yangu aliyo niteulia Mwenyezi Mungu niishike.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Simoore: Simoore heefereeɓe
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo saawaahiliiwo - Ali Muhsin Al-barwaany - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawahili, firi ɗum ko Ali Muhsin Al-barwani

Uddude