કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ * - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા


શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અલ્ મુર્સલાત   આયત:

Surat Al-Mursalat

وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa upepo unapovuma kwa mfululizo, huu baada ya huu.
અરબી તફસીરો:
فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا
Na kwa upepo wenye kuvuma kwa ukali wenye kuangamiza.
અરબી તફસીરો:
وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا
Na kwa Malaika waliopewa jukumu la mawingu, wakawa wayapeleka pale anapotaka Mwenyezi Mungu.
અરબી તફસીરો:
فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا
Na kwa Malaika wanaoshuka, kutoka kwa Mwenyezi Mungu,
અરબી તફસીરો:
فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا
na amri zinazopambanua baina ya haki na batili na halali na haramu.
અરબી તફસીરો:
عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا
Na kwa Malaika wanaoupokea wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kuuteremsha kwa Manabii Wake, unaowapa viumbe wake udhuru kutoka kwa Mwenyezi Mungu na pia onyo kutoka Kwake, ili watu wasiwe na hoja.
અરબી તફસીરો:
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ
Hakika jambo la Kiyama mnaloahidiwa pamoja na lile la kuhesabiwa na kulipwa ni lenye kuwa hapana shaka.
અરબી તફસીરો:
فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ
Basi nyota zitakapofutwa na mwangaza wake ukaondoka,
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ
na mbingu zitakapopasuka,
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ نُسِفَتۡ
na majabali yatakapopeperuka na kukueanea huku na kule na yakawa ni mapepe yanayorushwa na upepo,
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتۡ
Na Mitume watapowekewa wakati na muda wa baina yao na ummah wao na kusemwe,
અરબી તફસીરો:
لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ
«Ni Siku kubwa gani Mitume wameahirishiwa?»
અરબી તફસીરો:
لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ
Wameahirishiwa Siku ya hukumu na uamuzi baina ya viumbe.
અરબી તફસીરો:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ
Na nilipi lililokujulisha wewe, ewe binadamu, ni siku gani hiyo ya kutolewa uamuzi na ni zipi shida zake na vituko vyake?
અરબી તફસીરો:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu makubwa Siku hiyo ni ya wale waliyoikanusha Siku hii iliyoahidiwa.
અરબી તફસીરો:
أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ
Kwani hatukuawaangamiza walitangulia kati ya umma waliopita kwa kuwakanusha kwao Mitume, kama vile watu wa Nūḥ, ‘Ād na Thamūd?
અરબી તફસીરો:
ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ
Kisha tutawakutanisha na wao wale waliokuja nyuma kati ya wale waliokuwa ni kama wao katika ukanushaji na uasi.
અરબી તફસીરો:
كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ
Mfano wa uangamizaji huo mkali ndivyo tutakavyowafanya wahalifu kati ya makafiri wa Makkah, kwa kumkanusha kwao Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
અરબી તફસીરો:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa kila mwenye kuukanusha upweke wa Mwenyezi Mungu, unabii, kufufuliwa na kuhesabiwa.
અરબી તફસીરો:
أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ
Je kwani sisi hatukuwaumba nyinyi, enyi mkusanyiko wa makafiri, kutokana na maji dhaifu yaliyo matwevu nayo ni tone la manii,
અરબી તફસીરો:
فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ
tukayaweka maji haya kwenye mahali palipohifadhika, napo ni kizazi cha mwanamke,
અરબી તફસીરો:
إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ
mpaka kipindi maalumu kinachojulikana na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka?
અરબી તફસીરો:
فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ
Tukaweza kumuumba, kumtia sura na kumtoa. Basi bora wa wenye kuweza ni s isi.
અરબી તફસીરો:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kukanusha uweza wetu.
અરબી તફસીરો:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا
Je kwani hatukuifanya hii ardhi mnayoishi juu yake
અરબી તફસીરો:
أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا
ikusanye juu ya mgongo wake walio hai wasiohesabika, na ndani ya matumbo yake wafu wasiodhibitika, na
અરબી તફસીરો:
وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا
tukajaalia iwe na majabali yaliyojikita yaliyo marefu ili isitikisike na nyinyi, na tukawanywesha maji tamu yaliyo mazuri?
અરબી તફસીરો:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa waliozikanusha neema hizi.
અરબી તફસીરો:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Wataambiwa makafiri Siku ya Kiyama, «Endeni kwenye adhabu ya moto wa Jahanamu mliokuwa mkiukanusha duniani.
અરબી તફસીરો:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ
Endeni mjifinike kwenye kivuli cha moshi wa moto wa Jahanamu ambacho hapo panachembuka vipande vitatu.
અરબી તફસીરો:
لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ
Kivuli hiko hakimfanyi mtu ahifadhike na joto la Siku hiyo wala hakizuii muwako wa Moto chochote.
અરબી તફસીરો:
إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ
Hakika moto wa Jahanamu unarusha macheche makubwa ya moto, kila cheche moja katika hayo ni kama jengo lililoimarishwa katika ukubwa na urefu wa kuenda juu.
અરબી તફસીરો:
كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ
Kama kwamba hizo cheche za moto wa Jahanamu zinazopaa juu ni ngamia weusi ambao rangi yao imeingia kwenye umanjano.»
અરબી તફસીરો:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali kwa wenye kukanusha mateso yaliyoahidiwa na Mwenyezi Mungu.
અરબી તફસીરો:
هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ
Hii ndiyo Siku ya Kiyama ambayo wakanushaji hawatatamka maneno ya kuwanufaisha
અરબી તફસીરો:
وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ
wala hawatapewa idhini ya kusema wakatoa nyudhuru, kwa kuwa hawatakuwa na udhuru wowote.
અરબી તફસીરો:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali kwa wenye kuikanusha siku hii na yaliyomo ndani yake.
અરબી તફસીરો:
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ
Hii ni Siku ambayo Mwenyezi Mungu Atatoa uamuzi baina ya viumbe, na ukweli na ubatilifu utapambanuka. Tutawakusanya nyinyi Siku hiyo, enyi makafiri wa ummah huu, pamoja na makafiri wa mwanzo miongoni mwa ummah waliopita.
અરબી તફસીરો:
فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ
Basi mkiwa na hila za kujitoa na adhabu, tumieni hila zenu na mziokoe nafsi zenu na msukosuko wa Mwenyezi Mungu na mateso Yake.
અરબી તફસીરો:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya Kiyama.
અરબી તફસીરો:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ
Hakika ya wale waliomuogopa Mola wao duniani na wakaiogopa adhabu Yake kwa kufuata amri Zake na kujiepusha na makatazo Yake. Wao Siku ya Kiyama watakuwa kwenye vivuli vya miti vilivyonyoka, na chemchemi za maji zinazotembea,
અરબી તફસીરો:
وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ
na matunda mengi yanayopendwa na nafsi zao ambayo wao wanastarehe nayo. Hapo waambiwe,
અરબી તફસીરો:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
«Kuleni chakula chenye ladha na mnyweni kinywaji chenye kufurahisha kwa sababu ya matendo mema mliyoyatanguliza duniani.»
અરબી તફસીરો:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Sisi, kwa mfano wa malipo hayo makubwa, tutawalipa watu wema katika matendo yao na utiifu wao kwetu.
અરબી તફસીરો:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya Malipo na Hesabu, na kuzikanusha sterehe na mateso yaliyomo Siku hiyo.
અરબી તફસીરો:
كُلُواْ وَتَمَتَّعُواْ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجۡرِمُونَ
Kisha Mwenyezi Mungu Akawaonya makafiri kwa kusema, «Kuleni aina ya vyakula vya ladha duniani na stareheni kwa matamanio yake yenye kumalizika kwa muda mchache, hakika nyinyi ni wahalifu kwa kumshirikisha kwenu Mwenyezi Mungu.»
અરબી તફસીરો:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya kuhesabiwa na kulipwa.
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرۡكَعُواْ لَا يَرۡكَعُونَ
Na wanapoambiwa hawa washirikina, «Mswalieni Mwenyezi Mungu na mnyenyekeeni,» hawanyenyekei wala hawaswali, bali wanaendelea kuonyesha kiburi chao.
અરબી તફસીરો:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuzikanusha aya za Mwenyezi Mungu.
અરબી તફસીરો:
فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ
Iwapo wao hawataiamini hii Qur’ani, basi wataamini kitabu gani na maneno gani baada yake? Na Qur’ani yenyewe ni Kitabu kilichobainisha kila kitu, kilicho wazi katika hekima zake, hukumu zake na habari zake, chenye kushinda katika matamko yake na maana yake.
અરબી તફસીરો:
 
શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અલ્ મુર્સલાત
સૂરહ માટે અનુક્રમણિકા પેજ નંબર
 
કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા

સ્વાહિલી ભાષામાં કુરઆન મજીદનું ભાષાતર, ભાષાતર કરનારનું નામ અદ્ દૂકતુર અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અબૂ બકર અને શેખ નાસીર ખમીસ

બંધ કરો