કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ * - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા


શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અન્ નબા   આયત:

Surat An-Naba

عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
Kuhusu kitu gani baadhi ya makafiri wa Kikureshi wanaulizana?
અરબી તફસીરો:
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلۡعَظِيمِ
Wanaulizana kuhusu habari iliyo na uzito mkubwa kabisa,
અરબી તફસીરો:
ٱلَّذِي هُمۡ فِيهِ مُخۡتَلِفُونَ
nayo ni Qur’ani tukufu inayotoa habari za kufufuliwa ambako makafiri wa Kikureshi wana shaka nako na wanakukanusha.
અરબી તફસીરો:
كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Mambo sivyo kama wanavyodhania hawa washirikina. Hapo watajua hawa washirikina upeo wa kukanusha kwao na kitawadhihirikia waziwazi kile Atakachowatenda Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama.
અરબી તફસીરો:
ثُمَّ كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Kisha litahakikishika kwao jambo hilo na utahakikishika kwao ukweli wa yale aliyokuja nayo Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kuhusu Qur’ani na kufufuliwa. Huu ni utisho na makemeo kwao.
અરબી તફસીરો:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَٰدٗا
Kwani hatukuwatandazia ardhi kama tandiko?
અરબી તફસીરો:
وَٱلۡجِبَالَ أَوۡتَادٗا
Na Tukawafanyia majabali kuwa ni vigingi, ili isitisike nanyi?
અરબી તફસીરો:
وَخَلَقۡنَٰكُمۡ أَزۡوَٰجٗا
Na Tukawaumba aina mbali-mbali, mume na mke.
અરબી તફસીરો:
وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتٗا
Na Tukafanya usingizi wenu ni mapumziko kwa viwiliwili vyenu: ndani yake mnatulia na kupumzika?
અરબી તફસીરો:
وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسٗا
Na Tukaufanya usiku kuwa ni vazi, unawavisha giza lake na kuwafinika, kama nguo inavyomsitiri mwenye kuivaa.
અરબી તફસીરો:
وَجَعَلۡنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشٗا
Na Tukaufanya mchana ni kipindi cha kutafuta maisha, mnaenea humo kwa ajili ya maisha yenu na mnatembea humo kwa ajili ya maslahi yenu?
અરબી તફસીરો:
وَبَنَيۡنَا فَوۡقَكُمۡ سَبۡعٗا شِدَادٗا
Na Tukajenga juu yenu mbingu saba, madhubuti jengo lake, lilioumbwa kwa uzuri, halina mapasuko wala nyufa?
અરબી તફસીરો:
وَجَعَلۡنَا سِرَاجٗا وَهَّاجٗا
Na Tukalifanya jua kuwa ni taa iwakayo na kung’ara?
અરબી તફસીરો:
وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡمُعۡصِرَٰتِ مَآءٗ ثَجَّاجٗا
Na Tukateremsha kutoka kwenye mawingu yanyeshayo maji yamiminikayo kwa wingi,
અરબી તફસીરો:
لِّنُخۡرِجَ بِهِۦ حَبّٗا وَنَبَاتٗا
ili Tutoe kwa maji hayo nafaka inayoliwa na watu,
અરબી તફસીરો:
وَجَنَّٰتٍ أَلۡفَافًا
nyasi zinazoliwa na wanyama na miti iliyosongamana kwa kutawanyika tagaa zake?
અરબી તફસીરો:
إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ كَانَ مِيقَٰتٗا
Hakika Siku ya Uamuzi kati ya viumbe,
અરબી તફસીરો:
يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِ فَتَأۡتُونَ أَفۡوَاجٗا
nayo ni Siku ya Kiyama, imekuwa ni wakati na ahadi iliyowekewa muda maalimu kwa watu wa mwanzo na wa mwisho.
અરબી તફસીરો:
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٰبٗا
Na zikafunguliwa mbingu zikawa ni zenye milango mingi kwa ajili ya kuteremka Malaika.
અરબી તફસીરો:
وَسُيِّرَتِ ٱلۡجِبَالُ فَكَانَتۡ سَرَابًا
Na yakalipuliwa majabali baada ya kuwa yamekita, yakawa ni kama mangati.
અરબી તફસીરો:
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا
Hakika Jahanamu, Siku Hiyo, itawalindiza wenye ukafiri ambao Moto huo umeandaliwa wao.
અરબી તફસીરો:
لِّلطَّٰغِينَ مَـَٔابٗا
Kwa makafiri ndio marejeo.
અરબી તફસીરો:
لَّٰبِثِينَ فِيهَآ أَحۡقَابٗا
Watabakia humo muda mrefu ufuatanao, usiokoma.
અરબી તફસીરો:
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرۡدٗا وَلَا شَرَابًا
Hawatakula humo chochote kitakachozizimisha joto la moto kwao.
અરબી તફસીરો:
إِلَّا حَمِيمٗا وَغَسَّاقٗا
Wala kinywaji kitakachowaondolea kiu yao. Isipokuwa maji moto na usaha wa watu wa motoni.
અરબી તફસીરો:
جَزَآءٗ وِفَاقًا
Watakuwa wanalipwa kwa hilo malipo ya sawa yanayolingana na vitendo vyao walivyovitenda duniani
અરબી તફસીરો:
إِنَّهُمۡ كَانُواْ لَا يَرۡجُونَ حِسَابٗا
Hakika wao walikuwa hawaiyogopi Siku ya Hesabu, na kwa hivyo hawakujitayarisha nayo kwa kufanya matendo ya kuwafaa.
અરબી તફસીરો:
وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابٗا
Na waliyakanusha waziwazi yaliyoletwa na Mitume.
અરબી તફસીરો:
وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ كِتَٰبٗا
Na kila kitu Tulikijua na Tukakiandika katika Ubao uliohifadhiwa (Al-Lawḥ Al-Maḥfūd).
અરબી તફસીરો:
فَذُوقُواْ فَلَن نَّزِيدَكُمۡ إِلَّا عَذَابًا
Basi Onjeni, enyi makafiri, hayo yakiwa ni malipo ya vitendo vyenu, Hatutawazidishia isipokuwa adhabu juu ya adhabu yenu.
અરબી તફસીરો:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا
Hakika kwa wale ambao wanamuogopa Mola wao na huku wanatenda mema kuna kufaulu kwa kuingia Peponi.
અરબી તફસીરો:
حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا
Hakika watapata Mabustani makubwa na zabibu.
અરબી તફસીરો:
وَكَوَاعِبَ أَتۡرَابٗا
Na watapata wanawake wenye umri mdogo, wenye vifua vilivyojaza, marika na waume zao.
અરબી તફસીરો:
وَكَأۡسٗا دِهَاقٗا
Na watapata glasi zlizojaa pombe.
અરબી તફસીરો:
لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا كِذَّٰبٗا
Hawatasikia katika Pepo hiyo maneno ya upotofu wala kudanganyana.
અરબી તફસીરો:
جَزَآءٗ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابٗا
Watayapata yote hayo yakiwa ni malipo na zawadi na kipewa kingi cha kuwatosha kutoka kwa Mwenyezi Mungu,
અરબી તફસીરો:
رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلرَّحۡمَٰنِۖ لَا يَمۡلِكُونَ مِنۡهُ خِطَابٗا
Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati ya hizo, Mwenye kuwarehemu duniani na Akhera. Hawataweza kumuomba isipokuwa kile walichopewa ruhusa kumuomba.
અરબી તફસીરો:
يَوۡمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ صَفّٗاۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنۡ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَقَالَ صَوَابٗا
Siku atakaposimama Jibrili na Malaika wengine hali ya kujipanga mlolongo. Hawatamuombea isipokuwa yule aliyetolewa ruhusa na Mwingi wa Rehema ya kuombewa na akasema maneno ya haki na ya sawa.
અરબી તફસીરો:
ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلۡحَقُّۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Hiyo ndiyo siku ya haki isiyokuwa na shaka kuja kwake. Kwa hivyo, yule atakaye kuokoka na vituko vya Siku hiyo, na ajifanyie njia ya marejeo kwa Mola wake kutenda vitendo vyema.
અરબી તફસીરો:
إِنَّآ أَنذَرۡنَٰكُمۡ عَذَابٗا قَرِيبٗا يَوۡمَ يَنظُرُ ٱلۡمَرۡءُ مَا قَدَّمَتۡ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلۡكَافِرُ يَٰلَيۡتَنِي كُنتُ تُرَٰبَۢا
Sisi Tunawaonya nyinyi adhabu ya Siku ya mwisho iliyo karibu. Siku ambayo atayaona kila mtu aliyoyatenda katika kheri au aliyoyachuma miongoni mwa madhambi. Na kafiri atasema, kwa kitisho cha Hesabu, «Laiti mimi nilikuwa mchanga na sikufufuliwa.»
અરબી તફસીરો:
 
શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અન્ નબા
સૂરહ માટે અનુક્રમણિકા પેજ નંબર
 
કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા

સ્વાહિલી ભાષામાં કુરઆન મજીદનું ભાષાતર, ભાષાતર કરનારનું નામ અદ્ દૂકતુર અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અબૂ બકર અને શેખ નાસીર ખમીસ

બંધ કરો