કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ * - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા


શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અત્ તકવીર   આયત:

Surat At-Takwir

إِذَا ٱلشَّمۡسُ كُوِّرَتۡ
Pindi jua litakapokunjwa, na mwangaza wake ukaondoka.
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتۡ
Na pindi nyota zitakapopuputika na nuru yake ikafutika.
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ سُيِّرَتۡ
Na pindi majabali yatakapoondoshawa kwenye uso wa ardhi yakawa ni vumbi linaloenea.
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلۡعِشَارُ عُطِّلَتۡ
Na pindi ngamia wenye mimba watakapoachwa na kupuuzwa.
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلۡوُحُوشُ حُشِرَتۡ
Na pindi wanyama mwitu watakapokusanywa na kutangamanishwa, ili Mwenyezi Mungu Awape nafasi ya kulipizana wao kwa wao.
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ سُجِّرَتۡ
Na pindi bahari zitakapowashwa moto zikawa ni moto unaowaka.
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتۡ
Na pindi nafsi zitakapokutanishwa na mfano wake na sampuli yake.
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلۡمَوۡءُۥدَةُ سُئِلَتۡ
Na pindi mtoto wa kike aliyezikwa akiwa hai atakapoulizwa, Siku ya Kiyama, suala la kumbembeleza na kumkejeli aliyemzika:
અરબી તફસીરો:
بِأَيِّ ذَنۢبٖ قُتِلَتۡ
ni kwa dhambi gani ilikuwa kuzikwa kwake?
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتۡ
Na pindi kurasa za matendo zitakapoonyeshwa.
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتۡ
Na pindi mbingu zitakapong’olewa na kuondoshwa zilipokuwa.
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلۡجَحِيمُ سُعِّرَتۡ
Na pindi Moto utakapowashwa na ukawaka.
અરબી તફસીરો:
وَإِذَا ٱلۡجَنَّةُ أُزۡلِفَتۡ
Na pindi Pepo , Nyumba ya Neema, itakaposongezewa watu wake wachamungu.
અરબી તફસીરો:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّآ أَحۡضَرَتۡ
Litakapotokea hilo, itayakinisha kila nafsi na kujua kile ilichokitanguliza cha kheri au shari.
અરબી તફસીરો:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلۡخُنَّسِ
Anaapa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa nyota zinazofichika nuru yake mchana,
અરબી તફસીરો:
ٱلۡجَوَارِ ٱلۡكُنَّسِ
zinazotembea na zinazoghibu katika anga zake.
અરબી તફસીરો:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا عَسۡعَسَ
Na Anaapa kwa usiku unapojitokeza na giza lake.
અરબી તફસીરો:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Na kwa asubuhi unapojitokeza mwangaza wake.
અરબી તફસીરો:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Hakika Qur’ani ni ujumbe wa mjumbe mtukufu , naye ni Jibrili, amani imshukike.
અરબી તફસીરો:
ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي ٱلۡعَرۡشِ مَكِينٖ
Mwenye nguvu katika kuyapitisha yale anayoamrishwa. Mwenye cheo cha juu kwa Mwenyezi Mungu. Anayesikilizwa na Malaika.
અરબી તફસીરો:
مُّطَاعٖ ثَمَّ أَمِينٖ
Anayeaminiwa juu ya Wahyi anaoteremka nao.
અરબી તફસીરો:
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجۡنُونٖ
Hakuwa Muhammad mnayemjua ni mwendawazimu.
અરબી તફસીરો:
وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ
Na kwa hakika Muhammad alimuona Jibrili anayemjia na utume katika pambizo kubwa.
અરબી તફસીરો:
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ
Wala yeye hafanyi ubakhili katika kufikisha Wahyi.
અરબી તફસીરો:
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ
Wala haikuwa hii Qur’ani ni neno la Shetani aliyefukuzwa na kutolewa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu. Lakini Qur’ani hii ni maneno ya Mwenyezi Mungu na ni Wahyi wake.
અરબી તફસીરો:
فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ
Akili zenu zawapeleka wapi katika kukanusha baada ya hoja hizi zilizo wazi na zenye nguvu?
અરબી તફસીરો:
إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Hayakuwa haya isipokuwa ni mawaidha kutoka kwa Mwenyezi Mungu yanapewa watu wote.
અરબી તફસીરો:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ
Kwa atakaye, kati yenu, kulingana juu ya haki na Imani.
અરબી તફસીરો:
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala nyinyi hamtotaka isipokuwa kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote.
અરબી તફસીરો:
 
શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અત્ તકવીર
સૂરહ માટે અનુક્રમણિકા પેજ નંબર
 
કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા

સ્વાહિલી ભાષામાં કુરઆન મજીદનું ભાષાતર, ભાષાતર કરનારનું નામ અદ્ દૂકતુર અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અબૂ બકર અને શેખ નાસીર ખમીસ

બંધ કરો