કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ * - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા


શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અલ્ બલદ   આયત:

Surat Al-Balad

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mji huu mtakatifu wa Makkah.
અરબી તફસીરો:
وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Na wewe, ewe Nabii, ni mkazi wa mji huu mtakatifu.
અરબી તફસીરો:
وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ
Na Anaapa kwa mzazi wa wanaadamu, ambaye ni Ādam, amani imshukie, na kilichozalikana na yeye.
અરબી તફસીરો:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ
Hakika Tumemuumba binadamu katika usumbufu na shida za kilimwengu.
અરબી તફસીરો:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ
Kwani anadhani kwa mali aliyoyakusanya kuwa Mwenyezi Mungu Hatakuwa na uwezo juu yake?
અરબી તફસીરો:
يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا
Huwa akisema kwa kujigamba: «Nimetumia mali mengi.»
અરબી તફસીરો:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Kwani anadhani, kwa kitendo chake hiko, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda, Hamuoni wala hatamhesabu juu ya kubwa na dogo?
અરબી તફસીરો:
أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ
Kwani hatukumpa macho mawili ya kuonea,
અરબી તફસીરો:
وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ
ulimi na midomo miwili ya kusemea
અરબી તફસીરો:
وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ
na kumfafanulia njia mbili: ya kheri na ya shari?
અરબી તફસીરો:
فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ
Basi ajiepushe na janga la Akhera kwa kutoa mali yake ili aokoke.
અરબી તફસીરો:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ
Ni kitu gani kilichojulisha ni lipi hilo janga la Akhera na ni mambo gani yenye kusaidia kujiepusha nalo?
અરબી તફસીરો:
فَكُّ رَقَبَةٍ
Ni kuacha huru shingo iliyoamini kuikomboa na utumwa.
અરબી તફસીરો:
أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ
Au kulisha, wakati wa shida ya njaa,
અરબી તફસીરો:
يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ
yatima mwenye ujamaa, ili ipatikane fadhila ya sadaka na ya kuunga kizazi,
અરબી તફસીરો:
أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ
au masikini asiyekuwa na kitu.
અરબી તફસીરો:
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ
Kisha akawa, baada ya kufanya amali njema zilizotajwa, ni miongoni mwa waliotakasa Imani yao kwa Mwenyezi Mungu, wakausiana kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu kwa kufuata maamrisho Yake na kujiepusha na vitendo vya kumuasi na wakausiana kuwahurumia viumbe.
અરબી તફસીરો:
أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Wenye kufanya hayo ndiwo watu wa kulia ambao watapelekwa Siku ya Kiyama upande wa kulia kuelekea Peponi.
અરબી તફસીરો:
وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Na wale waliokanusha Qur’ani ndio ambao watapelekwa, Siku ya Kiyama, upande wa kushoto kuelekea Motoni.
અરબી તફસીરો:
عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ
Malipo yao ni Moto wa Jahanamu wenye kuwafinika na kuwaziba.
અરબી તફસીરો:
 
શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અલ્ બલદ
સૂરહ માટે અનુક્રમણિકા પેજ નંબર
 
કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા

સ્વાહિલી ભાષામાં કુરઆન મજીદનું ભાષાતર, ભાષાતર કરનારનું નામ અદ્ દૂકતુર અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અબૂ બકર અને શેખ નાસીર ખમીસ

બંધ કરો