क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस * - अनुवादों की सूची


अर्थों का अनुवाद आयत: (7) सूरा: सूरा आले इम्रान
هُوَ ٱلَّذِيٓ أَنزَلَ عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ مِنۡهُ ءَايَٰتٞ مُّحۡكَمَٰتٌ هُنَّ أُمُّ ٱلۡكِتَٰبِ وَأُخَرُ مُتَشَٰبِهَٰتٞۖ فَأَمَّا ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِمۡ زَيۡغٞ فَيَتَّبِعُونَ مَا تَشَٰبَهَ مِنۡهُ ٱبۡتِغَآءَ ٱلۡفِتۡنَةِ وَٱبۡتِغَآءَ تَأۡوِيلِهِۦۖ وَمَا يَعۡلَمُ تَأۡوِيلَهُۥٓ إِلَّا ٱللَّهُۗ وَٱلرَّٰسِخُونَ فِي ٱلۡعِلۡمِ يَقُولُونَ ءَامَنَّا بِهِۦ كُلّٞ مِّنۡ عِندِ رَبِّنَاۗ وَمَا يَذَّكَّرُ إِلَّآ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَٰبِ
Yeye Peke Yake Ndiye Ambaye Aliyekuteremshia Qur’ani ambayo katika hiyo kuna aya zenye maana yaliyo wazi; hizo ndizo msingi wa Kitabu ambao unategemewa ikitokea tashwishi, na ambao chochote kinachohalifiana nao kinarudishwa na kuoanishwa nao. Na katika hiyo kuna aya zingine mutashabihat: zinazoleta tashwishi kwa kuwa zinabeba zaidi ya maana mamoja, kwa namna ambayo haiwezekani kujuwa maana iliyokusudiwa isipokuwa kwa kuziambatanisha na muhkam: aya zenye maana yaliyo wazi. Basi wenye nyoyo zenye ugonjwa zilizopotoka, kwa ubaya wa nia zao, huzifuata hizi aya zenye tashwishi peke yake, ili kutia tashwishi kwa watu kwa lengo la kuwapoteza kwa kuzifasiri kuambatana na madhehebu yao yaliyo batili. Ilihali hakuna ajuwaye uhakika wa maana ya aya hizi isipokuwa Mwenyezi Mungu. Na wale waliovama kwenye elimu wanasema, «Tumeiamini hii Qur’ani, kwani yote imetujia kutoka kwa Mola wetu kwa ulimi wa Mtume Wake Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,.» na wanairudisha yenye tashwishi katika Qur’ani na kuiyoanisha na iliyo wazi yake. Hakika ni kwamba wanaoyafahamu na kuyazingatia maana kama ilivyo sahihi ipasavyo ni wale wenye akili timamu.
अरबी तफ़सीरें:
 
अर्थों का अनुवाद आयत: (7) सूरा: सूरा आले इम्रान
सूरों की सूची पृष्ठ संख्या
 
क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस - अनुवादों की सूची

पवित्र क़ुरआन के अर्थों का सवाहिली अनुवाद, अनुवादक : डॉ. अब्दुल्लाह मुहम्मद अबू बक्र तथा शैख़ नासिर ख़मीस

बंद करें