क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस * - अनुवादों की सूची


अर्थों का अनुवाद आयत: (73) सूरा: सूरा अल्-अन्आम
وَهُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۖ وَيَوۡمَ يَقُولُ كُن فَيَكُونُۚ قَوۡلُهُ ٱلۡحَقُّۚ وَلَهُ ٱلۡمُلۡكُ يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِۚ عَٰلِمُ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِۚ وَهُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡخَبِيرُ
Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa pungufu ni Kwake, Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi kwa haki. Na taja,ewe Mtume, Atakaposema Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama, «Kuwa» na ikawa kulingana na amri Yake, kama kupepesa macho au muda mfupi zaidi. Neno lake Ndio haki iliokamilika. Na ni Wake ufalme, Peke Yake, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, Siku Malaika atakapovuvia Parapanda, mvuvio wa pili ambao, kwa huo, roho zitarudi kwenye miili. Na Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni kwake, Ndiye Anayeyajua yaliyofichika na hisi zenu, enyi watu, mnayoyaona kwa macho yenu. Yeye Ndiye Mwenye hekima, Anayeweka mambo mahali pake, Mtambuzi wa mambo ya viumbe Vyake. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Ndiye Anayehusika na mambo haya na mengineyo, mwanzo na mwisho, kuanzisha kuumba na ukomo wake. Na Yeye, Peke Yake, Ndiye Ambaye inapasa kwa waja kufuata sheria Yake, kujisalimisha kwa hukumu Yake na kuwa nahamu ya kupata radhi Zake na msamaha Wake.
अरबी तफ़सीरें:
 
अर्थों का अनुवाद आयत: (73) सूरा: सूरा अल्-अन्आम
सूरों की सूची पृष्ठ संख्या
 
क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस - अनुवादों की सूची

पवित्र क़ुरआन के अर्थों का सवाहिली अनुवाद, अनुवादक : डॉ. अब्दुल्लाह मुहम्मद अबू बक्र तथा शैख़ नासिर ख़मीस

बंद करें