क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस * - अनुवादों की सूची


अर्थों का अनुवाद आयत: (108) सूरा: सूरा अत्-तौबा
لَا تَقُمۡ فِيهِ أَبَدٗاۚ لَّمَسۡجِدٌ أُسِّسَ عَلَى ٱلتَّقۡوَىٰ مِنۡ أَوَّلِ يَوۡمٍ أَحَقُّ أَن تَقُومَ فِيهِۚ فِيهِ رِجَالٞ يُحِبُّونَ أَن يَتَطَهَّرُواْۚ وَٱللَّهُ يُحِبُّ ٱلۡمُطَّهِّرِينَ
Usisimame, ewe Nabii, kuswali katika msikiti huo kabisa. Kwani msikiti uliojengwa kwa misingi ya uchamungu kuanzia siku ya mwanzo, nao ni msikiti wa Qubā’, unafaa zaidi kwa wewe kusimama humo kwa kuswali. Kwani katika msikiti huu kuna watu wanapenda kujisafisha na najisi na uchafu kwa maji, kama wanavyojisafisha kwa kujiepusha na mambo yanayopelekea kufanya mambo yaliyoharamishwa na kuomba msamaha kutokana na madhambi na maasia. Na Mwenyezi Mungu Anawapenda wenye kujisafisha.Na iwapo msikiti wa Qubā’ ulijengwa juu ya misingi ya uchaji-Mungu, basi Msikiti wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ni kama hivyo kwa njia ya ubora zaidi na ustahiki zaidi.
अरबी तफ़सीरें:
 
अर्थों का अनुवाद आयत: (108) सूरा: सूरा अत्-तौबा
सूरों की सूची पृष्ठ संख्या
 
क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस - अनुवादों की सूची

पवित्र क़ुरआन के अर्थों का सवाहिली अनुवाद, अनुवादक : डॉ. अब्दुल्लाह मुहम्मद अबू बक्र तथा शैख़ नासिर ख़मीस

बंद करें