Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani * - Daftar isi terjemahan

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Terjemahan makna Surah: Surah At-Takwīr   Ayah:

Surat At-Takwir

إِذَا ٱلشَّمۡسُ كُوِّرَتۡ
Jua litakapo kunjwa!
Jua litakapo kunjwa na mwangaza wake ukafutwa,
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتۡ
Na nyota zikazimwa!
Na nyota ikazimwa nuru yao,
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ سُيِّرَتۡ
Na milima ikaondolewa!
Na milima ikaondoshwa hapo ilipo,
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِذَا ٱلۡعِشَارُ عُطِّلَتۡ
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
Na ambao wa kuchukua mimba wakaharibu mimba zao,
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِذَا ٱلۡوُحُوشُ حُشِرَتۡ
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa!
Na nyama mwitu wakusanywe kutoka vichakani mwao na mashimoni mwao, hawajijui hawajitambui kwa wingi wa kufazaika.
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ سُجِّرَتۡ
Na bahari zikawaka moto!
Na bahari zikawa zinawaka moto,
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتۡ
Na nafsi zikaunganishwa!
Na roho zikaunganishwa na viwiliwili vyao,
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِذَا ٱلۡمَوۡءُۥدَةُ سُئِلَتۡ
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa!
Na mtoto wa kike aliye zikwa hai, akaulizwa kwa kumliwaza yeye, na kumshutumu aliye mzika hai,
Tafsir berbahasa Arab:
بِأَيِّ ذَنۢبٖ قُتِلَتۡ
Kwa kosa gani aliuliwa?
Kwa makosa gani kauliwa, naye hana dhambi? (Ilikuwa ada ya makafiri wa Kiarabu kabla ya Uislamu kuwazika watoto wao wa kike nao wahai! Baadhi ya Mabaniani wanawauwa watoto wao wa kike hata hivi leo huko India!!)
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتۡ
Na madaftari yatakapo enezwa,
Na nyaraka zilizo andikwa ndani vitendo vya watu zikakunjuliwa wakati wa hisabu.
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتۡ
 Na mbingu itapo tanduliwa,
Na mbingu itapo ondoshwa pahala pake,
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِذَا ٱلۡجَحِيمُ سُعِّرَتۡ
Na Jahannamu itapo chochewa,
Na Moto ukawashwa kwa mwako mkali,
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِذَا ٱلۡجَنَّةُ أُزۡلِفَتۡ
Na Pepo ikasogezwa,
Na Pepo ikajongezwa ikawa karibu,
Tafsir berbahasa Arab:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّآ أَحۡضَرَتۡ
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
Yatakapo tokea yote hayo, basi hapo tena kila nafsi itajua nini iliyo tanguliza, ikiwa kheri au shari.
Tafsir berbahasa Arab:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلۡخُنَّسِ
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
Naapa kiapo cha mkazo kwa nyota ambazo zinanywea zinapo chomoza, na hapo mwanga wake huwa khafifu,
Tafsir berbahasa Arab:
ٱلۡجَوَارِ ٱلۡكُنَّسِ
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
Zenye kwenda na hujificha wakati wa kuchwa kwake, kama paa wanapo jificha kwenye mapango yao.
Tafsir berbahasa Arab:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا عَسۡعَسَ
Na kwa usiku unapo pungua,
Na kwa usiku linapo pungua giza lake wakati unapo malizika.
Tafsir berbahasa Arab:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
Na kwa asubuhi unapo anza mwangaza wake na ukavuma upepo wake,
Tafsir berbahasa Arab:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
Hakika Qur'ani bila ya shaka ni kauli ya Mjumbe anaye toka kwa Mwenyezi Mungu, naye ni mwenye kuhishimiwa kwake,
Tafsir berbahasa Arab:
ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي ٱلۡعَرۡشِ مَكِينٖ
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
Mwenye nguvu katika kutekeleza waajibu wake, mwenye cheo na daraja mbele ya Mwenyezi Mungu Mwenye Kiti cha Enzi.
Tafsir berbahasa Arab:
مُّطَاعٖ ثَمَّ أَمِينٖ
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
Tena ni mwenye kut'iiwa, na muaminifu wa kuchukua wahyi miongoni wa walio juu.
Tafsir berbahasa Arab:
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجۡنُونٖ
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
Na huyo Mtume wenu ambaye ni mwenzenu, mnaye mjua kuwa ana akili timamu, si mwendawazimu.
Tafsir berbahasa Arab:
وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
Na ninaapa kuwa Muhammad s.a.w. bila ya shaka alimwona Jibrili katika upeo wa macho kwa mujibu wa inavyo onekana.
Tafsir berbahasa Arab:
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
Na Muhammad si bakhili wa kufikisha wahyi na kuwafunza watu.
Tafsir berbahasa Arab:
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
Wala huu wahyi (ufunuo) ulio teremshwa juu yake si kauli ya Shetani aliye fukuzwa kutoka kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu.
Tafsir berbahasa Arab:
فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ
Basi mnakwenda wapi?
Basi njia gani iliyo ya uwongofu zaidi kuliko hii mnayo ifuata?
Tafsir berbahasa Arab:
إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
Qur'ani si chochote ila ni ukumbusho na mawaidha kwa walimwengu wote.
Tafsir berbahasa Arab:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
Kwa anaye taka, miongoni mwenu, kusimama sawa kufikilia haki na kweli.
Tafsir berbahasa Arab:
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Na nyinyi hamwezi kutaka kitu ila anapo taka Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Surah: Surah At-Takwīr
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani - Daftar isi terjemahan

Terjemahan Makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke Bahasa Sawahili oleh Ali Muhsin Al-Barwani

Tutup