Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis * - Indice Traduzioni


Traduzione dei significati Sura: Ash-Shams   Versetto:

Surat Ash-Shams

وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa jua na mchana wake na mwangaza wake wa asubuhi.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Na kwa mwezi unapolifuata wakati wa kucha na kutwa.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Na kwa mchana unapoliondoa giza na kulifunua.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا
Na kwa usiku unapoifinika ardhi ikawa giza.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Na kwa mbingu na kujengeka kwake kiimara.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Na kwa ardhi na kutandikika kwake.
Esegesi in lingua araba:
وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا
Na kwa kila nafsi na namna Mwenyezi Mungu alivyoikamilisha umbo lake ili itekeleze kazi iliyoumbiwa nayo.
Esegesi in lingua araba:
فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا
Akaibainishia njia ya shari na njia ya kheri.
Esegesi in lingua araba:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Amefaulu mwenye kuisafisha na kuikuza kwa kheri.
Esegesi in lingua araba:
وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Na ameingia kwenye hasara mwenye kuitia nafsi yake kwenye maasia.
Esegesi in lingua araba:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ
Kabila la Thamūd lilimkanusha Nabii wake kwa kuvama kwenye uasi.
Esegesi in lingua araba:
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا
Pindi walipotoka wabaya zaidi wa kabila hilo kumchinja Ngamia. Mtume wa Mwenyezi Mungu’ Ṣāliḥ, amani imshukie,
Esegesi in lingua araba:
فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا
akawaambia: «Tahadharini kumgusa kwa ubaya ngamia ambaye ni miujiza ilioletwa na Mwenyezi Mungu kwenu inayoonyesha ukweli wa Nabii wenu, na msizuie kinywaji chake. Yeye ana siku yake ya kunywa na nyinyi mna siku yenu maalumu ya kunywa.» Hilo likawa zito kwao.
Esegesi in lingua araba:
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا
Wakamkanusha na kulipuza onyo lake wakamchinja.Mola wao Akawafinika kwa adhabu, akaisawazisha juu yao na hakuna aliyeweza kuponyoka.
Esegesi in lingua araba:
وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا
Wala Haogopi, Mwenye uwezo uliotukuka, athari ya adhabu kali Aliywateremshia.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Sura: Ash-Shams
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Abdullah Mohammed ِAbu Bakr e Shaikh Nasser Khamis

Chiudi