Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany * - Indice Traduzioni

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduzione dei significati Sura: Al-Humazah   Versetto:

Surat Al-Humazah

وَيۡلٞ لِّكُلِّ هُمَزَةٖ لُّمَزَةٍ
Ole wake kila safihi, msengenyaji!
Atapata adhabu kali na maangamio huyo ambaye mtindo wake ni kuwafedhehi watu kwa kauli au kwa ishara, au kuwasengenya kuwavunjia hishima zao.
Esegesi in lingua araba:
ٱلَّذِي جَمَعَ مَالٗا وَعَدَّدَهُۥ
Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
Ambaye amekusanya chungu ya mali na akawa kazi yake kuyahisabu tu, kwa kuona ladha huko kuhisabu.
Esegesi in lingua araba:
يَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخۡلَدَهُۥ
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
Anadhani huyo kuwa mali yake yatamweka milele duniani, na yatamkinga na hayo anayo yachukia?
Esegesi in lingua araba:
كَلَّاۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِي ٱلۡحُطَمَةِ
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.
Na aache dhana hiyo! Wallahi! Hapana shaka yoyote kwa vitendo vyake viovu hivyo atakuja tumbukizwa katika Moto unao vuruga kila kinacho tupwa humo!
Esegesi in lingua araba:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحُطَمَةُ
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?
Na kitu gani kitacho kujuvya nini ukweli wa Moto huu wa H'ut'ama?
Esegesi in lingua araba:
نَارُ ٱللَّهِ ٱلۡمُوقَدَةُ
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa kwa amri yake, na daima unawaka!
Esegesi in lingua araba:
ٱلَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى ٱلۡأَفۡـِٔدَةِ
Ambao unapanda nyoyoni.
Ambao unafikilia nyoyoni na kuzizunguka nyoyo.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّهَا عَلَيۡهِم مُّؤۡصَدَةٞ
Hakika huo utafungiwa nao
Huo utakuwa umefungwa milango yake, na wao watakuwa wamefungwa humo ndani
Esegesi in lingua araba:
فِي عَمَدٖ مُّمَدَّدَةِۭ
Kwenye nguzo zilio nyooshwa.
Kwenye maguzo yaliyo nyooka. Hawawezi kutaharaki, wala kutoka.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Sura: Al-Humazah
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Ali Muhsin Albirwany

Chiudi