クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis * - 対訳の目次


対訳 章: 包まる者章   節:

Surat Al-Muddathir

يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُدَّثِّرُ
Ewe uliojifinika nguo zako!
アラビア語 クルアーン注釈:
قُمۡ فَأَنذِرۡ
Inuka kutoka kwenye malazi yako owaonye watu adhabu ya Menyezi Mungu.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَرَبَّكَ فَكَبِّرۡ
Na umkusudie Mola wako, Peke Yake, kwa kumtukuza, kumpwekesha na kumuabudu.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَثِيَابَكَ فَطَهِّرۡ
Na usafishe nguo zako kutokana na najisi, kwani usafi wa nje ni katika kutimia usafi wa ndani.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَٱلرُّجۡزَ فَٱهۡجُرۡ
Na uendelee daima kuyaepuka masanamu na mizimu, na matendo ya ushirikina yote usiyakaribie.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَلَا تَمۡنُن تَسۡتَكۡثِرُ
Na usitoe kitu kumpa mtu kwa lengo la kupata zaidi ya hiko. Na kwa ajili ya kupata radhi ya Mwenyezi Mungu,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَلِرَبِّكَ فَٱصۡبِرۡ
vumilia juu ya maamrisho na makatazo.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَإِذَا نُقِرَ فِي ٱلنَّاقُورِ
Pindi patakapopulizwa kwenye barugumu mpulizo wa Ufufuzi na Uenezaji,
アラビア語 クルアーン注釈:
فَذَٰلِكَ يَوۡمَئِذٖ يَوۡمٌ عَسِيرٌ
wakati huo ni wakati ambao ni mgumu kwa makafiri;
アラビア語 クルアーン注釈:
عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ غَيۡرُ يَسِيرٖ
si rahisi kwao kusalimika na yale walionayo ya kujadiliwa hesabu zao na vituko vingine vikubwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
ذَرۡنِي وَمَنۡ خَلَقۡتُ وَحِيدٗا
Niache mimi, ewe Mtume, na huyu niliyemuumba ndani ya tumbo la mamake akiwa peke yake, hana mali wala watoto.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَجَعَلۡتُ لَهُۥ مَالٗا مَّمۡدُودٗا
Nikamfanya awe na mali mengi yenye kuenea na watoto waliyoko na yeye hapo Makkah hawamuondokei. Na
アラビア語 クルアーン注釈:
وَبَنِينَ شُهُودٗا
nikamsahilishia kwa kumrahisishia njia za maisha. Kisha yeye anatarajia, baada ya vitu hivi alivyopewa,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمۡهِيدٗا
nimuongezee kwenye mali yake na watoto wake na huku yeye amenikanusha. Mambo sivyo kama anavyodai huyu mwenye kuasi, mtenda dhambi.
アラビア語 クルアーン注釈:
ثُمَّ يَطۡمَعُ أَنۡ أَزِيدَ
Simuongezei zaidi ya hiko nilichompa,
アラビア語 クルアーン注釈:
كَلَّآۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِأٓيَٰتِنَا عَنِيدٗا
kwa kuwa yeye alikuwa mshindani mkanushaji wa Qur’ani na hoja za Mwenyezi Mungu kwa viumbe Wake.
アラビア語 クルアーン注釈:
سَأُرۡهِقُهُۥ صَعُودًا
Nitambebesha mateso magumu na usumbufu usio na mapumziko. Anayekusudiwa hapa ni Al-Walid mwana wa Al-Mughi rah aliyekuwa akishindana na haki na akijitokeza kupigana vita na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Haya ndiyo malipo ya kila mwenye kushindana na haki na kuipiga vita.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ
Kwa kweli yeye aliwaza ndani ya nafsi yake akatayarisha la kusema kumtukana Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Hivyo basi akalaaniwa na akastahili, kwa hilo, maangamivu: alijiandaa vipi ndani ya nafsi yake kwa hayo matukano?
アラビア語 クルアーン注釈:
ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Kisha pia akalaaniwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
ثُمَّ نَظَرَ
Kisha yeye alifikiria kuhusu kile alichokipanga na kukitayarisha cha kuitia dosari Qur’ani.
アラビア語 クルアーン注釈:
ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ
Kisha akafinya uso wake na akazidi katika hali ile ya ukunjaji uso kwa kukosa hila za kufanya na kutopata ila yoyote ya kuitia dosari Qur’ani.
アラビア語 クルアーン注釈:
ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ
Kisha akarudi kuipa mgongo haki na akajiona ni mkubwa wa kutofaa kuikubali,
アラビア語 クルアーン注釈:
فَقَالَ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ يُؤۡثَرُ
hapo akasema kuhusu Qur’ani, «Haya anayoyasema Muhammad si chochote isipokuwa ni uchawi uliopokewa kutoka kwa watu wa mwanzo waliopita.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا قَوۡلُ ٱلۡبَشَرِ
Haikuwa hi Qur’ani isipokuwa ni maneno ya viumbe ambayo Muhammad amejifunza kutoka kwao kisha akadai kuwa yanatoka kwa Mwenyezi Mungu.»
アラビア語 クルアーン注釈:
سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ
Basi nitamuingiza kwenye moto wa Jahanamu ili alionje joto lake na achomeke kwa moto wake.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ
Na ni lipi lililokujulisha wewe ni kitu gani hiyo Jahanamu?
アラビア語 クルアーン注釈:
لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ
Haibakishi nyama wala haiachi mfupa isipokuwa huvichoma.
アラビア語 クルアーン注釈:
لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ
Unageuza ngozi ya mwili, unazifanya ngozi kuwa nyeusi na unazichoma.
アラビア語 クルアーン注釈:
عَلَيۡهَا تِسۡعَةَ عَشَرَ
Wanasimamia mambo yake na kushikilia kazi ya kuwatesa watu wake Malaika kumi na tisa katika washika zamu wa Motoni wenye nguvu.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ
Na hatukuwafanya washika hazina wa Motoni isipokuwa miongoni mwa Malaika washupavu. Na hatukuiweka idadi hiyo isipokuwa kuwatahini wale waliomkufuru Mwenyezi Mungu, na ili imani ya yakini ipatikane kwa wale Mayahudi na Wanaswara waliopewa Vitabu kwamba yaliyokuja ndani ya Qur’ani juu ya washika hazina wa Motoni ni ukweli utokao kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, kwani hayo yanaafikiana na vitabu vyao, na ili Waumini wazidi kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na waifuate Sheria Yake kivitendo, na ili wasilifanyie shaka hilo wale Mayahudi na Wanaswara waliopewa Vitabu wala wale wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na ili wapate kusema wale wenye unafiki ndani ya nyoyo zao na makafiri, «Ni lipi alilolikusudia Mwenyezi Mungu kwa idadi hii ya ajabu?» Kwa mfano wa hayo yaliyotajwa, Mwenyezi Mungu Anampoteza Anayetaka kumpoteza na Anamuongoza Anayetaka kumuongoza. Na hakuna ajuwaye idadi ya askari wa Mola wako, na miongoni mwao ni Malaika, isipokuwa Mwenyezi Mungu Peke Yake. Na haukuwa huu Moto isipokuwa ni ukumbusho na mazingatio kwa watu.
アラビア語 クルアーン注釈:
كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ
Mambo sivyo kama walivyotaja ya ukanushaji Mtume katika yale aliyokuja nayo! Anaapa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kila sifa ya upungufu, kwa mwezi,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ
na kwa usiku unapogeuka kwenda zake,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ
na kwa asubuhi inapotoa mwangaza na kufunuka,
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ
hakika Moto ni mojawapo ya mambo makubwa,
アラビア語 クルアーン注釈:
نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ
kwa ajili ya kuwaonya na kuwatisha watu,
アラビア語 クルアーン注釈:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ
kwa anayetaka miongoni mwenu kujiweka karibu na Mola wake kwa kufanya matendo ya utiifu, au kujikalisha nyuma kwa kufanya matendo ya uasi.
アラビア語 クルアーン注釈:
كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ
Kila nafsi imefungwa na kuwekwa rahani kwa ilichokitenda, miongoni mwa matendo mema au mabaya, kwa kukichuma. Haifunguliwi mpaka itekeleze haki zilizo juu ya lazima yake na ipatiwe mateso yanayostahili kupatiwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ
Isipokuwa Waislamu waliotakaswa, watu wa upande wa kulia waliojikomboa shingo zao kwa utiifu.
アラビア語 クルアーン注釈:
فِي جَنَّٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ
Wao watakuwa kwenye mabustani ya Peponi ambayo sifa zake hazifikiwi ukomo. Watakuwa wakiulizana wao kwa wao
アラビア語 クルアーン注釈:
عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
kuhusu makafiri waliojikosea nafsi zao,
アラビア語 クルアーン注釈:
مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ
«Ni lipi lililowaingiza kwenye moto wa Jahanamu na likawafanya
アラビア語 クルアーン注釈:
قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ
mlionje joto lake lililo kali sana?» Wahalifu waseme , «Hatukuwa ni miongoni mwa wanaoswali duniani,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ
na hatukuwa tukitoa sadaka na kuwafanyia wema wahitaji na maskini,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ
na tulikuwa tukizungumza maneno ya ubatilifu na watu wa upotofu na upotevu,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
na tulikuwa tukiikanusha Siku ya kuhesabiwa na kulipwa,
アラビア語 クルアーン注釈:
حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ
mpaka kifo kikatujia na hali sisi tuko kwenye mambo hayo mabaya ya upotevu.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَمَا تَنفَعُهُمۡ شَفَٰعَةُ ٱلشَّٰفِعِينَ
Basi hayatawafalia neno maombezi ya wenye kuombea wote, miongoni mwa Malaika, Manabii na wengineo, kwa kuwa aombewaye ni yule aliyechaguliwa na Mwenyezi Mungu na akamuidhinisha mwenye kumuombea.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَمَا لَهُمۡ عَنِ ٱلتَّذۡكِرَةِ مُعۡرِضِينَ
Basi wana nini hawa washirikina wamejiepusha na Qur’ani na
アラビア語 クルアーン注釈:
كَأَنَّهُمۡ حُمُرٞ مُّسۡتَنفِرَةٞ
mawaidha yaliyomo ndani yake? Kama kwamba wao ni pundamilia wanaobabaika
アラビア語 クルアーン注釈:
فَرَّتۡ مِن قَسۡوَرَةِۭ
wanaomkimbia simba mshambulizi.
アラビア語 クルアーン注釈:
بَلۡ يُرِيدُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُؤۡتَىٰ صُحُفٗا مُّنَشَّرَةٗ
Lakini kila mmoja, miongoni mwa hawa washirikina, ana matumaini ateremshiwe kitabu kutoka mbinguni kilichokunjuliwa kama kile kilichoteremshiwa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
アラビア語 クルアーン注釈:
كَلَّاۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Mambo si hivyo kama wanavyodai. Ukweli ni kwamba wao hawaiogopi Akhera wala hawaamini kuwa kuna kufufuliwa na kulipwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذۡكِرَةٞ
Ni kweli kwamba Qur’ani ni mawaidha yenye ufasaha, yanayotosha kuwafanya wao wawaidhike.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Anayetaka kuwaidhika, basi na awaidhike kwa yaliyomo ndani yake na anufaike na uongofu wake.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَمَا يَذۡكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ هُوَ أَهۡلُ ٱلتَّقۡوَىٰ وَأَهۡلُ ٱلۡمَغۡفِرَةِ
Na hawawaidhiki kwayo isipokuwa iwapo Mwenyezi Mungu Amewatakia kuongoka. Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Anayestahiki kuogopewa na kutiiwa, na Ndiye Anayestahiki kumsamehe anayemuamini Yeye na kumtii.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 章: 包まる者章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

閉じる