クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis * - 対訳の目次


対訳 章: 復活章   節:

Surat Al-Qiyamah

لَآ أُقۡسِمُ بِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Siku ya Hesabu na Malipo,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلنَّفۡسِ ٱللَّوَّامَةِ
na Anaapa kwa nafsi yenye kuamini na kuchamungu, inayomlaumu mwenyewe kwa kuacha matendo ya utiifu na kufanya matendo yenye kuangamiza, kwamba watu watafufuliwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجۡمَعَ عِظَامَهُۥ
Je anadhanihuyu binadamu kafiri kuwa sisi hatutaweza kuikusanya mifupa yake baada ya kuwa mbalimbali.?
アラビア語 クルアーン注釈:
بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُۥ
Ndio! Tutaikusanya na tunaweza kufanya vidole vyake au ncha za vidole vyake- baada ya kuvikusanya na kuzioanisha- viwe kwenye umbo la sawasawa, kama vilivyokuwa kabla ya kufa.
アラビア語 クルアーン注釈:
بَلۡ يُرِيدُ ٱلۡإِنسَٰنُ لِيَفۡجُرَ أَمَامَهُۥ
Bali binadamu anakanusha kufufuliwa, anataka asalie kwenye kufanya ubaya kwa siku za mbeleni za maisha yake.
アラビア語 クルアーン注釈:
يَسۡـَٔلُ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Kafiri huyu huwa akiuliza, akiliona jambo la kusimama Kiyama kuwa liko mbali, «Ni lini Siku ya Kiyama?’
アラビア語 クルアーン注釈:
فَإِذَا بَرِقَ ٱلۡبَصَرُ
Basi macho yatakapoduwaa na yakashituka kwa kutishika na kile yalichokiona cha vituko vya Siku ya Kiyama,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَخَسَفَ ٱلۡقَمَرُ
na ukafutika mwangaza wa mwezi,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَجُمِعَ ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ
na vikakusanywa jua na mwezi katika kukosa mwangaza, kikawa kila mojawapo ya hivyo viwili hakina mwangaza,
アラビア語 クルアーン注釈:
يَقُولُ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذٍ أَيۡنَ ٱلۡمَفَرُّ
wakati huo binadamu atasema, «Pa kukimbilia ni wapi kuiepuka adhabu?»
アラビア語 クルアーン注釈:
كَلَّا لَا وَزَرَ
Mambo sivyo kama unavyotamani yawe, ewe binadamu, ya kutaka kukimbia. Huna mahali pa kukimbilia wala pa kupata uokozinfsi yake.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمُسۡتَقَرُّ
Kwa Mwenyezi Mungu Peke Yake ndio mwisho wa viumbe Siku ya Kiyama na ndipo mahali pao pa kutulia, na hapo Amlipe kila mtu kwa kile alichostahiki.
アラビア語 クルアーン注釈:
يُنَبَّؤُاْ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذِۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
Atapashwa habari binadamu Siku hiyo kwa matendo yake yote, mema na mabaya, aliyoyatanguliza miongoni mwa hayo katika maisha yake na aliyoyachelewesha.
アラビア語 クルアーン注釈:
بَلِ ٱلۡإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٞ
Bali binadamu ni hoja iliyo wazi juu ya nafsi yake, yenye kumfuata kwa alichokitenda na alichokiacha,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ
hata kama atakuja na kila udhuru wa kuelezea sababu ya uhalifu wake, hilo halitamfaa.
アラビア語 クルアーン注釈:
لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ
Usitikise, ewe Nabii, ulimi wako kwa Qur’ani wakati wahyi unapoteremka ili ufanye haraka kuihifadhi kwa kuogopa isikuponyoke.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ
Kwani ni juu yetu sisi kuikusanya kwenye kifua chako kisha uisome kwa ulimi wako wakati utakapo. Mjumbe wetu Jibrili akikusomea,
アラビア語 クルアーン注釈:
فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ
basi kisikilize kisomo chake na umpulikize. Kisha isome kama alivyokusomea,
アラビア語 クルアーン注釈:
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ
kisha ni juu yetu kukuelezea kilichokutatiza kukifahamu katika maana yake na hukumu zake.
アラビア語 クルアーン注釈:
كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ
Mambo sivyo kama mlivyodai, enyi mkusanyiko wa washirikina, kuwa hakuna kufufuliwa wala kulipwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Bali nyinyi ni watu mnaopenda dunia na pambo lake na mnaacha Akhera na starehe zake.
アラビア語 クルアーン注釈:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ
Nyuso za watu wema Siku ya Kiyama zitakuwa ni zenye kung’ara, nzuri na zenye furaha,
アラビア語 クルアーン注釈:
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ
zitamuona Mola Aliyeziumba na Anayezimiliki, na zitastarehe kwa hilo.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ
Nyuso za watu wabaya Silku ya Kiyama zitakuwa ni zenye kukunjana na kusinyaa,
アラビア語 クルアーン注釈:
تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ
zinatazamia kushukiwa na msiba mkubwa wenye kuvunja.
アラビア語 クルアーン注釈:
كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ
Ni kweli! Pindi roho itakapofika sehemu za juu za kifua,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ
na wakasema baadhi ya waliohudhuria kuwaambia wengine, «Je kuna mtu wa kumzungua na kumpoza kutokana na hali hii aliyonayo?»
アラビア語 クルアーン注釈:
وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ
Na yule ambaye yuko katika hali ya kufa akajua kwamba lile lililomshukia ni kuaga dunia, kwa kuwa anawaona Malaika wa mauti.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ
Na ikashikana shida ya mwisho wa duniani na shida ya mwanzo wa Akhera. Kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ
Watu watapelekwa Siku ya Kiyama: ima Peponi au Motoni.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
Hakuwa kafiri ni mwenye kumuamini Mtume na Qur’ani, wala hakuwa ni mwenye kumtekelezea Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Swala za faradhi.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Lakini aliikanusha Qur’ani na akaipa mgongo Imani,
アラビア語 クルアーン注釈:
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ
kisha akaenda kwa watu wake akijiona hali ya kujigamba katika kutembea kwake. Basi maangamivu
アラビア語 クルアーン注釈:
أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ
ni yako baada ya maangamivu!
アラビア語 クルアーン注釈:
ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ
Kisha maangamivu ni yako baada ya maangamivu!
アラビア語 クルアーン注釈:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى
Je anadhani huyu binadamu anayekanusha kufufuliwa kuwa ataachwa bure: haamrishwi wala hakatazwi, hahesabiwi wala hateswi?
アラビア語 クルアーン注釈:
أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ
Kwani hakuwa binadamu huyu ni tone la manii dhaifu linalotokana na maji matwevu yanayomwagwa na kumiminwa kwenye kizazi,
アラビア語 クルアーン注釈:
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
kisha yakawa ni kipande cha damu iliyo kavu. Mwenyezi Mungu Akaliumba kwa uweza Wake na Akazilinganisha sura zake katika umbo la mwili lililo zuri kabisa?
アラビア語 クルアーン注釈:
فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Akafanya kutokana na binadamu huyu jinsi mbili: ya kiume na ya kike. Je kwani hakuwa Mola huyo Muumba wa vitu hivyo ni Muweza wa kuwarudisha viumbe wakiwa hai baada ya kutoweka kwao.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ
Ndio! Anaweza. Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, kwa hakika ni Muweza wa hilo.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 章: 復活章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

閉じる