クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis * - 対訳の目次


対訳 章: 凝血章   節:

Surat Al-Alaq

ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ
Soma, ewe Nabii, Qur’ani uliyoteremshiwa ukianza kwa Jina la Mola wako Aliyepwekeka kwa kuumba.
アラビア語 クルアーン注釈:
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ
Aliyemuumba kila binadamu kwa pande la damu nzito nyekundu.
アラビア語 クルアーン注釈:
ٱقۡرَأۡ وَرَبُّكَ ٱلۡأَكۡرَمُ
Soma, ewe Nabii, kile ulichoteremshiwa, na Mola wako ni Mwingi wa wema, Mwingi wa ukarimu.
アラビア語 クルアーン注釈:
ٱلَّذِي عَلَّمَ بِٱلۡقَلَمِ
Aliyewafundisha viumbe vyake kuandika kwa kalamu.
アラビア語 クルアーン注釈:
عَلَّمَ ٱلۡإِنسَٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ
Alimfundisha binadamu vitu ambavyo hakuwa akivijua. Akamtoa kwenye giza la ujinga, Akampeleka kwenye nuru ya elimu.
アラビア語 クルアーン注釈:
كَلَّآ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَيَطۡغَىٰٓ
Kweli, binadamu hukiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu
アラビア語 クルアーン注釈:
أَن رَّءَاهُ ٱسۡتَغۡنَىٰٓ
akijiona ametosheka kwa utajiri wake.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجۡعَىٰٓ
Basi, ajue kila mwenye kutupa mipaka kuwa mwisho atarudi kwa Mwenyezi Mungu Ambaye Atamlipa kila binadamu kwa alilolitenda.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يَنۡهَىٰ
Je, umeona ujeuri wa ajabu zaidi kuliko wa mtu huyu, Abu jahl,
アラビア語 クルアーン注釈:
عَبۡدًا إِذَا صَلَّىٰٓ
Anayemkataza mja wetu, Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, anapomsalia Mola wake?
アラビア語 クルアーン注釈:
أَرَءَيۡتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلۡهُدَىٰٓ
Waonaje iwapo mwenye kukatazwa kusali yuko uongofuni, vipi anamkataza?
アラビア語 クルアーン注釈:
أَوۡ أَمَرَ بِٱلتَّقۡوَىٰٓ
Au iwapo anaamrisha mwigine kumcha Mungu, vipi anamkataza hilo?
アラビア語 クルアーン注釈:
أَرَءَيۡتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ
Waonaje iwapo huyu mwenye kukataza anakanusha lile alinganiwalo kwalo na kulipa mgongo,
アラビア語 クルアーン注釈:
أَلَمۡ يَعۡلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ
hajui kuwa Mwenyezi Mungu anaona kila analolifanya?
アラビア語 クルアーン注釈:
كَلَّا لَئِن لَّمۡ يَنتَهِ لَنَسۡفَعَۢا بِٱلنَّاصِيَةِ
Basi mambo si kama anvyodai Abu Jahl. Na asipokomeka na ushindani alionao na udhia wake, Tutamshika upaa wake kwa nguvu na kumtia Motoni.
アラビア語 クルアーン注釈:
نَاصِيَةٖ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٖ
Upaa wake ni upaa wenye maneno ya urongo na vitendo vya makosa.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَلۡيَدۡعُ نَادِيَهُۥ
Basi na awalete, mtupaji mipaka huyu, watu wa baraza ili wamsaidiye.
アラビア語 クルアーン注釈:
سَنَدۡعُ ٱلزَّبَانِيَةَ
Sisi Tutawaita Malaika wa adhabu.
アラビア語 クルアーン注釈:
كَلَّا لَا تُطِعۡهُ وَٱسۡجُدۡۤ وَٱقۡتَرِب۩
Mambo si kama Abu Jahl anavyoyadhania. Yeye, ewe Mtume, hawezi kukufanya lolote la kukudhuru Usimfuate kwa lile alilokuitia la kuwa uache Swala, bali msujudie Mola wako na uwe karibu na Yeye kwa kujipendekeza Kwake kwa kumtii.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 章: 凝血章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

閉じる